Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Lukuvi aanika aliyoyafanya ardhi toka 2014
Habari Mchanganyiko

Lukuvi aanika aliyoyafanya ardhi toka 2014

Wiliam Lukuvi, aliyekuwa Waziri wa Ardhi na Maendeleo ya Jamii
Spread the love

 

ALIYEKUWA Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, William Lukuvi, amesema miongoni mwa kazi kubwa alizozifanya tangu aliposhika wadhifa huo 2014, kukomesha vitendo vya matajiri na wenye madaraka kupora ardhi za wananchi wanyonge. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma…(endelea).

Mbunge huyo wa Isimani (CCM), ameyataja mafanikio hayo leo Alhamisi, tarehe 17 Februari 2022, akimkabidhi ofisi mrithi wake, Dk. Angelina Mabula, aliyeteuliwa na Rais Samia kuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, hivi karibuni.

“Wakati tunaingia 2014 tulikuwa na mambo mengi hapa, hata mheshimiwa Jakaya Kikwete (Rais wa wakati huo), alivyoniteua kuna mambo mengi alikuwa ameniambia. Lakini wakati ule kulikuwa na malalamiko makubwa ya dhulma katika wizara hii, tumeshirikiana angalau kukomesha dhulma Kwa taratibu mbalimbali,” amesema Lukuvi na kuongeza:

“Wananchi wengi walikuwa wanadhulumiwa ardhi yao na watu wenye pesa na madaraka, lakini tumejitahidi kupunguza angalau sasa hata malalmiko hayo yamepungua.”

Kwa upande wake Dk. Mabula, ameahidi kuendeleza pale alipoishia Lukuvi, ili kuendelea kuimarisha utendaji wa wizara hiyo katika kuwahudumia wananchi.

“Haya yote ambayo umeyazungumza tumeyafanya tukiwa pamoja, naomba nikuthibitishie tutayaendeleza. Kwa sababu ndiyo yaliyobadilisha sura ya wizara. Ilikuwa kwenye Bunge tukiingia wizara ya ardhi ni siku tatu lakini imefikia mahali mpaka nusu siku kazi inakuwa imekwisha,” amesema Dk. Mabula na kuongeza:

“Nitaomba Mungu anijaalie pamoja na timu hii tusirudi kule nyuma, mnapangiwa siku mbili au tatu za wizara. Kipi kinajadiliwa? Maana yake huku mtakuwa mmetekeleza kwamba sasa baada ya Lukuvi kutoka kuna mambo hayaendi sawa matokeo yake tunarudi tulikotoka.”

1 Comment

  • Asante sana ndugu lukuvi lakini kipindi chako ulwatoa thamani wanachi wa daraja la tatu na kuwapa thamani wawekezaji sehemu ambayo wanaishi watu wa daraja la tatu unawapa wawekezaji na kuwambia watu wadaraja waondoke na wataripwa wakiuliza sababu ya kuondoka unajibu muwekezaji anapataka wakiuliza twende wapi na hapa ndio kwetu jibu ardhi mali ya umma wakiuliza sisi ndio umma mbona unatuambia tuondoke jibu tunataka maendeleo .kweli lukuvi maendeleo hayaji bira kuwa hamisha watu wa daraja la tatu katika makazi yao. Ndugu lukuvi wawekezaji hao wanapo itaji hao ni makazi ya watu wa daraja la tatu tu ostabey micochen and upanga wawekezaji hawapati ndugu lukuvi wizara ya ardhi inawapa mashaka makubwa wanachi wa daraja la tatu kila wanapo lala hawajui kesho itakuwaje wenzetu wa daraja la kwanza shaka hawana.serekali.wapen.thamani.kwanza wanachi wa daraja la tatu mwekezaj awe wa mwisho kwa thamani

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Gardner Habash wa Clouds Fm afariki dunia

Spread the loveALIYEKUWA mtangazaji wa kipindi cha Jahazi kinachorushwa na kituo cha...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

error: Content is protected !!