Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Lowassa amchokonoa Lissu
Habari za Siasa

Lowassa amchokonoa Lissu

Edward Lowassa
Spread the love

KITENDO cha Tundu Lissu, mgombea urais wa Tanzania, kupitia Chadema, kuonekana kwenye televisheni na kuzunguka majimboni wakati wa kampeni zake, kimebezwa na Edward Lowassa, aliyekuwa mgombea urais wa chama hicho mwaka 2015. Anaripoti Mwandishi Wetu, Monduli … (endelea).

Lowassa alijiunga na Chadema Jumanne tarehe 28 Julai 2015, akiambatana na familia yake, katika mkutano na waandishi wa habari uliofanyika katika Hoteli ya Bahari Beach jijini Dar es Salaam.

Leo tarehe 24 Septemba 2020 amesema “Lissu ana maneno mengi, fujo.’

Akizungumza kwenye kikao cha ndani cha Chama Cha Mapinduzi (CCM), Monduli jijini Arusha, Lowassa amemsifu aliyekuwa mpinzani wake mkubwa kwenye uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 Dk. John Magufuli, kwamba utawala wake umefanya makubwa.

Na kwamba, amemtaka Dk. Magufuli ambaye ni mgombea urais wa CCM kutokuwa na wasiwasi wa kushinda kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020.

“…huko kwa kina Lissu wameanza kujipambanua sana, maneno mengi, fujo zile, wanaonekana kwenye mamitaa, maTV (televisheni), matv mengine yanatishatisha, lakini tulimwambia rais wetu, usitishike hata kidogo,” amesema Lowassa kwenye kikao hicho.

Tundu Lissu, Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema

Lowassa ambaye alikuwa Waziri Mkuu katika Serikali ya awamu ya nne chini ya Rais mstaafu Jakaya Mrisho Kikwete, amesema, hana mashaka na ushindi wa Dk. Magufuli na kwamba, alicho na mashaka nacho ni idadi ya kura zake za ushindi.

“Mimi sina mashaka juu ya kushinda, mashaka yangu atapita kwa kura ngapi? amesema Lowassa akisisitiza kwamba, Watanzania wengi wanamuunga mkono.

“Umma wa Watanzania uko nyuma yako na dunia inajua kwamba kuna mwanaume Tanzania. Nasema hivyo kwa sababu, Australia kama ulisikiliza BBC leo, rais anajiuzulu, kule Bolivia rais anajiuzulu, yote kwa sababu ya hii kitu, corona si mchezo,” amesema Lowassa.

Katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015, Lowassa alipata kura milioni 6.07 sawa na asilimia 39.97 huku Dk. Magufuli akipata kura milioni 8.88 sawa na asilimia 58.46

Hata hivyo, Lowassa alirejea CCM tarehe 1 Machi 2019 na kupokewa na Dk. Magufuli ambaye ni mwenyekiti wa chama hicho, kwenye ofisi ndogo ya CCM Lumumba, jijini Dar es Salaam.

Wengine waliompokea Lowassa aliporejea CCM ni pamoja Philip Mangula (Makamu Mwenyekiti CCM-Bara), Dk. Bashiru Ally (Katibu Mkuu), Humphery Polepole (Katibu wa Itikadi na Uenezi), Kasim Majaliwa (Waziri Mkuu) na swahiba wake wa siku nyingi Rostam Aziz.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!