Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lowassa aitosa Chadema, arudi CCM
Habari za SiasaTangulizi

Lowassa aitosa Chadema, arudi CCM

Rais John Magufuli, Mwenyekiti wa CCM akimpokea Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa aliporejea CCM
Spread the love

WAZIRI Mkuu Mstaafu wa serikali ya awamu ya nne, Edward Lowassa amerejea CCM akitokea Chadema. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Lowassa amerejea CCM leo tarehe 1 Machi 2019 na kupokelewa na Katibu Mkuu wa chama hicho Dk. Bashiru Ally katika ofisi ndogo za CCM jijini Dar es Salaam.

Akizungumza baada ya kumpokea Lowassa, Dk. Bashiru ameeleza kuwa ujio wa mwanasiasa huyo mkongwe hapa nchini unaashiria kwamba chama hicho kinaanza kazi ya kujenga Taifa.

“Kama alivyosema Waziri Mkuu Mstaafu Lowasa amerudi nyumbani, tunaanza kazi ya kujenga taifa letu na kulinda udugu wetu ,” amesema Dk. Bashiru.

Lowassa alihama CCM katika vuguvugu la kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 baada ya kushindwa katika kura za maoni za kuwania nafasi ya kuipeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa urais, na kuipata fursa hiyo kupitia Chadema kwa mwamvuli wa vyama vinavyounda UKAWA.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Rais Samia ataja mikakati ya kufikia trilioni 2 biashara Uturuki, Tz

Spread the loveWakati Tanzania na Uturuki zikidhamiria kuongeza kiwango cha biashara hadi...

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

error: Content is protected !!