
Rais John Magufuli, Mwenyekiti wa CCM akimpokea Waziri Mkuu Mstaafu Edward Lowassa aliporejea CCM
WAZIRI Mkuu Mstaafu wa serikali ya awamu ya nne, Edward Lowassa amerejea CCM akitokea Chadema. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).
Lowassa amerejea CCM leo tarehe 1 Machi 2019 na kupokelewa na Katibu Mkuu wa chama hicho Dk. Bashiru Ally katika ofisi ndogo za CCM jijini Dar es Salaam.
Akizungumza baada ya kumpokea Lowassa, Dk. Bashiru ameeleza kuwa ujio wa mwanasiasa huyo mkongwe hapa nchini unaashiria kwamba chama hicho kinaanza kazi ya kujenga Taifa.
“Kama alivyosema Waziri Mkuu Mstaafu Lowasa amerudi nyumbani, tunaanza kazi ya kujenga taifa letu na kulinda udugu wetu ,” amesema Dk. Bashiru.
Lowassa alihama CCM katika vuguvugu la kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2015 baada ya kushindwa katika kura za maoni za kuwania nafasi ya kuipeperusha bendera ya chama hicho katika uchaguzi wa urais, na kuipata fursa hiyo kupitia Chadema kwa mwamvuli wa vyama vinavyounda UKAWA.
More Stories
Simba yabadilishiwa muda wa mechi Sudan, sasa kukipiga saa 9
Uchaguzi wa wanawake Chadema waingiliwa
Dk. Mwinyi amteua Dk. Mkuya, Nassor Mazrui