Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa ‘Lockdown’ siku ya Eid
Kimataifa

‘Lockdown’ siku ya Eid

Saudi Arabia
Spread the love

SIKU ya Sikukuu ya Eid el Fitr na siku nne mbele, wananchi wa Saudi Arabia wametangaziwa kutotoka nje. Utekelezaji wa tangazo hilo utaanzia tarehe 23 mpaka 27 Mei 2020. Inaripoti mitandao ya kimataifa … (endelea).  

Hatua hiyo imechukuliwa ili kuzia maambukizo mapya ya virusi vya corona (COVID-19), na kwamba watu hawatoruhusiwa kutoka nje kwa saa 24 katika siku zote tano.

Mpaka leo Jumatano tarehe 13 Mei 2020, taifa hilo lina maambukizo 42,925 vifo vikiwa 264 huku waliopona wakiwa 15,257.

Taarifa ya Suleyman Soylu, Waziri ya Mambo ya Ndani ya taifa hilo imeeleza, mpaka sasa biashara na shughuli zingine kwenye maeneo mbalimbali ya taifa hilo yanaendelea kama kawaida lakini kuanzia saa 3 asubuhi mpaka saa 11 jioni.

Wizara hiyo imesisitiza, pamoja na maeneo hayo kuwa huru kwa muda huo, wakazi wa Mji wa Makka wanaendelea kuwa ndani mpaka hapo tangazo lingine litapotolewa.

Makka ndio mji pekee katika taifa hilo uliofungwa, watu wake hawaruhusiwi kutoka ndani.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanaye rais jela miaka miaka 6 kwa dawa za kulevya

Spread the loveMwanawe rais wa zamani wa Guinea-Bissau amehukumiwa kifungo cha miaka...

Habari za SiasaKimataifa

Faye aahidi kuongoza kwa unyenyekevu, wagombea wenzie wakubali yaishe

Spread the loveMgombea wa upinzani Senegal, Bassirou Diomaye Faye anajiandaa kuwa rais...

Habari MchanganyikoKimataifa

Wanafunzi 130 waliokuwa wametekwa nyara waokolewa

Spread the loveZaidi ya wanafunzi 130 wa shule ya msingi LEA na...

Habari MchanganyikoKimataifa

Mgombea upinzani aongoza uchaguzi wa Rais Senegal

Spread the loveMgombea wa upinzani nchini Senegal, Bassirou Diomaye Faye ameonekana kuongoza...

error: Content is protected !!