Saturday , 20 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lijualikali aondoka Chadema, amwaga chozi kwa kunyanyaswa
Habari za SiasaTangulizi

Lijualikali aondoka Chadema, amwaga chozi kwa kunyanyaswa

Spread the love

MBUNGE wa Kilombero (Chadema), Peter Lijualikali, amejiondoa katika chama hicho. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).

Akizungumza bungeni Mjini Dodoma jioni ya leo, Lijualikali amesema, ameamua kuondoka Chadema kwa kuwa chama hicho, kinaendeshwa “kidikteta.”

Amesema, uamuzi wa chama chake kususuia mkutano wa Bunge kwa madai ya kujitenga na karatini, haukufuata taratibu.

Akiongea kwa uchungu huku akitokwa na machozi, Lijualikali amesema, amepitia makubwa na kwamba hawezi kubaki Chadema, kwa kuwa kuna mambo ya ajabu sana.

Amesema, wabunge wa Chadema wametawaliwa na woga, na hivyo kushindwa kumwambia kiongozi wa chama hicho, Freeman Mbowe kuwa unakosea.

Amemtuhumu Mbowe kutafuna baadhi ya fedha za chama hicho na kuongeza kuwa kila wanapotaka kuuliza, wanaambiwa hakuna kuhoji.

“Niko tayari kulima hata mpunga, kuendesha bodaboda na kufanya kazi nyingine yeyote. Niko tayari, lakini siko tayari kubaki Chadema,” ameeleza.

Lijualikali amesema yuko tayari kujiunga na Chama cha Mapinduzi (CCM) endapo kitakubali kumpokea na atakuwa tayari kufanya kazi yoyote ndani ya chama hicho

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MWANACHAMA wa Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Boniface Jacob, amedai...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!