Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Liverpool yabanwa mbavu
Michezo

Liverpool yabanwa mbavu

Spread the love

BINGWA mtetezi wa Ligi Kuu nchini England klabu ya Liverpool imelazimishwa sare ya mabao 2-2 dhidi ya Everton kwenye mchezo wa Ligi nchini humo uliochezwa majira ya saa 8 mchana kwenye Uwanja wa Goodson Park. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Liverpool imeambulia pointi moja katika michezo miwili ya Ligi kuu nchini humo mara baada ya kupoteza katika mchezo uliopita dhidi ya Astorn Villa.

Mabao ya Liverpool kwenye mchezo huo yalifungwa na Sadio Mane dakika ya 3 na Mohammed Salah 71’ ambaye amefikisha mabao 100 toka alipojiunga na Liverpool.

Kwa upande wa Everton mabao yao yalipatikana dakika ya 19 na Kean, na baadae dakika ya 81’ Calvert Lewin akaisawazishia timu yake na mchezo kumalizika sare.

Kwa matokeo hayo Liverpool itakuwa na alama 10 na kusogea nafasi ya pili huku Everton ikiendelea kusalia kileleni kwenye msimamo huo kwa kuwa na pointi 13 baada ya kucheza michezo mitano.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!