Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Liverpool, Manchester Kumaliza ‘kiporo’ chao leo
Michezo

Liverpool, Manchester Kumaliza ‘kiporo’ chao leo

Spread the love

 

 Mara baada ya mchezo wa Ligi Kuu nchini England kati ya Liverpool na Manchester United kuarishwa kutokana na vurugu za Mashabiki wa Manchester kuandamana, hatimaye wakongwe hao watakipiga leo kwenye Uwanja wa Old Trafford majira ya saa 4 usiku. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Wawili hao wanakutana huku tayari bingwa mpya ambaye ni klabu ya Manchester City ameshatangazwa, mara baada ya Manchester United kukubali kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Leceister City.

Mchezo huu ambapo utakuwa muhimu zaidi kwa Liverpool kutokana na kugombania nafasi nne za juu ili waweze kushiliki michuano ya Ligi yaMabingwa Barani Ulaya msimu ujao.

Liverpool ipo nafasi ya sita ikiwa na pointi 57, na michezo 34 huku nafasi ya tano ikishikwa na Westham ikiwa na pointi 58 na michezo 35.

Nafasi ya nne inakamatwa na Chelsea mwenye pointi 64 na michezo 36, huku kwenye nafasi ya tatu akishikilia Leceister City mwenye pointi 66 na michezo 36.

Mchezo huo ambapo hapo awali ulipangwa kuchezwa tarehe 5 Mei 2021 haukufanyika kutokana na maandamano waliyoyafanya mashabiki wa klabu ya Manchester United ambao walikuwa wanashinikiza kwa wamiliki wa timu hiyo Familia ya Glazzer kuachana na timu hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!