Tuesday , 3 October 2023
Home Kitengo Michezo Liverpool, Manchester Kumaliza ‘kiporo’ chao leo
Michezo

Liverpool, Manchester Kumaliza ‘kiporo’ chao leo

Spread the love

 

 Mara baada ya mchezo wa Ligi Kuu nchini England kati ya Liverpool na Manchester United kuarishwa kutokana na vurugu za Mashabiki wa Manchester kuandamana, hatimaye wakongwe hao watakipiga leo kwenye Uwanja wa Old Trafford majira ya saa 4 usiku. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Wawili hao wanakutana huku tayari bingwa mpya ambaye ni klabu ya Manchester City ameshatangazwa, mara baada ya Manchester United kukubali kichapo cha mabao 2-1 dhidi ya Leceister City.

Mchezo huu ambapo utakuwa muhimu zaidi kwa Liverpool kutokana na kugombania nafasi nne za juu ili waweze kushiliki michuano ya Ligi yaMabingwa Barani Ulaya msimu ujao.

Liverpool ipo nafasi ya sita ikiwa na pointi 57, na michezo 34 huku nafasi ya tano ikishikwa na Westham ikiwa na pointi 58 na michezo 35.

Nafasi ya nne inakamatwa na Chelsea mwenye pointi 64 na michezo 36, huku kwenye nafasi ya tatu akishikilia Leceister City mwenye pointi 66 na michezo 36.

Mchezo huo ambapo hapo awali ulipangwa kuchezwa tarehe 5 Mei 2021 haukufanyika kutokana na maandamano waliyoyafanya mashabiki wa klabu ya Manchester United ambao walikuwa wanashinikiza kwa wamiliki wa timu hiyo Familia ya Glazzer kuachana na timu hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

UEFA imekuja na maokoto yakutosha bashiri na Meridianbet sasa

Spread the love UTAMU wa kubeti ule bhana, na ukitaka kula ni...

BiasharaMichezo

BetPawa kuwasaidia Watanzania 20 awamu ya 2 ‘Dream Maker’

Spread the loveKAMPUNI  ya michezo ya kubahatisha ya BetPawa Tanzania,  jana Jumatatu...

Michezo

Taswa wampongeza Mobhare Matinyi

Spread the love  CHAMA cha Waandishi wa Habari za Michezo Tanzania (TASWA),...

Michezo

Waziri madini atembelea banda la GGML, ashuhudia mradi wa uwanja wa kisasa

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde ametembelea banda la Kampuni ya...

error: Content is protected !!