CHAMA tawala nchini Tanzania- Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinafanya mkutano mkuu maalum leo Ijumaa tarehe 1 Aprili 2022 katika ukumbi wa Jakaya Kikwete jijini Dodoma…(endelea). Anaripoti Mwandishi Wetu, Dodoma … (endelea).
Mkutano huo unaongozwa na Mwenyekiti wake ambaye ni Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan ambao tayari umekwisha kuanza na kuhudhuriwa na wageni mbalimbali wa ndani na nje ya Taifa hilo.
Lengo la mkutano mkuu huo ni kufanya marekebisho ya Katiba ya CCM yam waka 1977 toleo la mwaka 2020 pamoja na kufanya uchaguzi wa Makamu Mwenyekiti wa CCM- Bara ambapo mgombea ni mmoja pekee, Abdulrahman Kinana.
Kinana anatarajiwa kurithi nafasi ya Philip Mangula ambaye jana Alhamisi, mbele ya kikao cha Halmashauri Kuu ya CCM alitangaza kung’atuka katika nafasi hiyo.
Fuatilia mkutano huo kupitia MwanaHALISI TV, MwanaHALISI Online na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali
Leave a comment