MKUTANO wa Baraza Kuu la chama kikuu cha upinzani nchini Tanzania cha Chadema unafanyika leo Jumatano tarehe 11 Mei 2022, katika ukumbi wa Mlimani City jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Anayeongoza mkutano huo ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe.
Pamoja na mambo mengine, baraza hilo litasikiliza rufaa za waliokuwa wanachama wao 19 akiwemo Halima Mdee ambap tarehe 27 Novemba 2020 walifukuzwa ndani ya chama hicho.
Walifukuzwa baada ya kutuhumiwa kqa usaliti, kughushi nyaraka za chama na kujipeleka bungeni kuapishwa kuwa wabunge wa viti maalum kinyume na taratibu za Chadema.
Kwa mujibu wa ratiba, agenda kuhusu rufaa hiyo ni ya mwisho kujadiliwa.
Mbali na Mdee aliyekuwa mwenyekiti wa baraza la wanawake wa Chadema (Bawacha), wengine ni, waliokuwa wajumbe wa Kamati Kuu, Ester Bulaya na Esther Matiko pamoja na aliyekuwa katibu mkuu wa Bawacha, Grace Tendega.
Pia wamo, Hawa Mwaifunga, aliyekuwa makamu mwenyekiti wa Bawacha (Bara); Agnesta Lambat, aliyekuwa katibu mwenezi na Asia Mwadin Mohamed, aliyekuwa naibu katibu mkuu wa Bawacha Zanzibar na Katibu Mkuu, Bawacha-Bara, Jesca Kishoa
Wengine ni, aliyekuwa katibu mkuu wa Baraza la Vijana (Bavicha), Nusrat Hanje, aliyekuwa mwenyekiti wa Chadema mkoani Mtwara, Tunza Malapo.
Cecilia Pareso, Naghenjwa Kaboyoka, Sophia Mwakagenda, Kunti Majala, Salome Makamba, Anatropia Theonest, Conchesta Lwamlaza, Felister Njau na Stella Siyao.
Leave a comment