Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa ‘Lissu ndiye amiri jeshi mkuu ajaye’
Habari za Siasa

‘Lissu ndiye amiri jeshi mkuu ajaye’

Salum Mwalimu, Mgombea Mwenza wa Urais Tanzania kwa tiketi ya Chadema
Spread the love

SALUM Mwalimu, mgombea mwenza wa urais kupitia Chama Cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Tundu Lissu ndiye amir jeshi mkuu ajaye. Anaripoti Christina Haule, Morogoro … (endelea).

 Amesema, Lissu kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika tarehe 28 Oktoba 2020, anakwenda kumshinda kwa kura nyingi mgombea urais wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. John Magufuli.

Akizungumza kwenye mkutano wake wa kampeni katika Viwanja vya Shujaa, Morogoro tarehe 29 Septemba 2020 amesema, watumishi wa umma na vyombo vya ulinzi na usalama ikiwemo Jeshi la Polisi, Magereza na Uhamiaji wajiandaye kisaikolojia kuongozwa na Chadema.

“Chadema hatuji na askari wetu, hatuna wanajeshi wetu wala watumishi wa umma tuliowaweka pembeni, tunakuja kutumia watumishi, jeshi haohao, kinachokwenda kubadilika ni jambo moja tu, kila aliyepo kwenye nafasi yake ahakikishe anatenda haki na kutoa uhuru kwa raia tunaokwenda kuwaongoza,” amesema.

Pia amesema tayari wamempa taarifa Dk. Magufuli kwamba hawana kinyongo naye, bali watamtunzia heshima yake kama Rais Mstaafu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!