Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu kurejea rasmi nchini Januari 25 baada ya miaka mitano uhamishoni
Habari za SiasaTangulizi

Lissu kurejea rasmi nchini Januari 25 baada ya miaka mitano uhamishoni

Tundu Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

 

MAKAMU Mwenyekiti wa Chadema Bara, Tundu Lissu ametangaza kurejea nchi rasmi tarehe 25, Januari, 2023 ikiwa ni zaidi ya miaka mitano ya kuwa ughaibuni nchini Ubelgiji. Anaripoti Mwandihi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Lissu ametoa taarifa hiyo leo Ijumaa tarehe 13 Januari 2023, katika hotuba yake ya salamu za mwaka mpya 2023 kwa watanzania.

Amesema uamuzi wa kurejea nchini ni baada ya maazimio ya Kamati Kuu ya chama chake kwamba kutokana na mabadiliko ya hali ya kisiasa nchi Lissu na wenzake waliopo ughaibuni warejee nchini.
Wanachama wengine wa Chadema waliopo ughaibuni ni mjumbe wa Kamati Kuu, Godbelss Lema aliyepo

Canada na Ezekiel Wenje. Wote waliondoka baada ya uchaguzi mkuu wa mwaka 2020 kwa kile walichoeleza kuwa maisha yao yalikuwa hatarini.

“Ukiondoa takribani miezi mitatu ya kipindi cha uchaguzi Mkuu Oktoba 2020 nimeishi uhamishoni kwa zaidi ya mitano kuanzia siku niliyokimbizwa Nairobi Kenya kwa matibabu ya dharura baada ya jaribio la mauji dhidi yangu la tarehe 7 Septemba 2017,” amesema Lissu na kuongeza;

“Hiki kimekuwa kipindi kirefu na kigumu sana katika maisha yangu binafsi na maisha yetu kama chama na kama Taifa.”

Hata hivyo Lissu ameeleza sababu kubwa ya kurejea nyumbani ni kuja kuendeleza kazi kubwa ya kutafuta Katiba Mpya.

“Ninarudi kwaajili ya kazi kubwa iliyopo mbele yetu, kazi ya Katiba Mpya na mwanzo mpya kwa Taifa letu, ninarudi nyumbani kuja kushiriki katika kuandika ukurasa wa kwanza mpya wa kitabu chenye kurasa 365 cha mwaka huu 2023,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!