Thursday , 7 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu katika tundu la sindano NEC
Habari za Siasa

Lissu katika tundu la sindano NEC

Tundu Lissu, Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema, akirudisha fomu ya kuteuliwa nafasi hiyo kwa Mwenyekiti wa NEC, Jaji Semistocles Kaijage
Spread the love

TUNDU Lissu, mgombe urais kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) na mgombea mwenza wake Salum Mwalimu, wameponea kwenye ‘tundu la sindano.’ Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Lissu, Mwalimu walijikuta wakitumia zaidi ya saa saba ndani ya Makao Makuu ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kutokana na fomu zao wakati wa uhakiki kubainika kuwa na kasoro.

Kwa mujibu wa taratibu za NEC, fomu za Lissu zilikosa baadhi ya vigezo vilivyohutajika kulingana na mahitaji ya taratibu za kupitishwa kugombea urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Fomu za Lissu ambaye pia ni Makamu Mwenyekiti wa Chadema, zilikosa uhakiki wa taarifa za wadhamini wake 2,000 kutoka kwenye mikoa 10 kama inavyoelekeza sheria ya uchaguzi.

Badala yake Lissu na chama chake walitaka fomu hizo zihakikiwe katika ofisi za NEC, tofauti na vyama vingine ambavyo wagombea wake walihakiki fomu zao mapema na sehemu husika.

Kwa mujibu wa ratiba ya NEC ya kurudisha fomu za uteuzi wa wagombea wa kiti cha urais na makamu wake, Chadema kilikuwa chama cha nne kwa wagombea wake kurudisha fomu, ambapo walipangiwa kuanza zoezi hilo saa 6:00 mchana hadi saa 6:15 mchana.

Lakini Chadema walifanikiwa kukabidhi fomu hizo saa moja kioni baada ya kukamilisha taratibu za uhakiki wa fomu. Zoezi la uhakiki wa fomu zao lilichukua takribani nusu saa ikilinganishwa na vyama vingine ambavyo vilitumia dakika 15 kulikamilisha.

Baada ya kukamilisha zoezi hilo, Jaji Semistocles Kaijage, Mwenyekiti wa NEC alimtangaza Lissu na Mwalimu kwamba, wameteuliwa kugombea nafasi hiyo baada ya kukidhi vigezo.

Uchaguzi Mkuu unatarajiwa kufanyika tarehe 28 Oktoba 2020, ambapo kwa mujibu wa kalenda ya NEC, kampeni zinaanza leo.

1 Comment

  • Nenda nyinyi vibaraka wa ccm
    Kwanza hukai hapa
    Pili wewe na Gwajima hanna tafauti
    Tatu sisi kura yetu twampa Mama Mdee

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bashungwa: Katesh kutafanyiwa usafi wa hali ya juu

Spread the loveWAZIRI wa Ujenzi, Innocent Bashungwa amesema kazi ya kuondoa tope...

AfyaHabari za Siasa

RAS Songwe: Tumepigwa… mkurugenzi nakupa siku 21

Spread the loveKATIBU tawala mkoani Songwe, Happines Seneda ametoa siku 21 kwa...

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

error: Content is protected !!