Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu atumia mtumbwi kuwafikia wapigakura
Habari za SiasaTangulizi

Lissu atumia mtumbwi kuwafikia wapigakura

Tundu Lissu, Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema akivuka Ziwa Victoria kwa kutumia kutumia mtumbwi akieleka Ukelewe
Spread the love

MSAFARA wa Tundu Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chadema umelazimika kutumia mtubwi kutoka Kisorya mkoani Mara kwenda Ukerewe Mkoa wa Mwanza. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mara … (endelea)

Leo Jumatano tarehe 14 Oktoba 2020, msafara wa Lissu walifika eneo hilo la Kisorya ili kwenda Ukerewe umbali unaokadiliwa kuwa kilomita 21.9 kuhutubia mkutano wa kampeni lakini, kivuko kinachotoa huduma eneo hilo kilielezwa ni kibovu.

Kwa mujibu wa rariba ya Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) inaonyesha mkutano wa kwanza Lissu anapaswa kuufanya Ukerewe kisha baadaye atakuwa Jimbo la Rorya Mkoa wa Mara.

 

Katika ukurasa wake wa Twitter, Lissu ameweka video wakiwa wanataka kuanza safari na kuandika “kwa mara ya pili katika kipindi hiki cha kampeni, bila sababu za msingi, hamna kivuko cha Kisorya kwa ajili ya msafara wetu kwenda Ukerewe.”

“Yote ni kwa ajili ya kuzuia tusifike huko. Sasa tutavuka kivingine na tutafanya mkutano kama ilivyo ratiba! Haturudi nyuma,” amesema Lissu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

error: Content is protected !!