Friday , 9 June 2023
Habari za SiasaTangulizi

Lissu atoa ya moyoni

Tundu Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema
Spread the love

TUNDU Lissu, Mbunge was Singida Mashariki amesema kuwa upinzani umeshambuliwa kuliko kipindi chochote nchini Tanzania. Anaripoti Yusuph Katimba … (endelea).

Lissu amesema hivyo leo tarehe 28 Agosti 2018 usiku saa 3:23 alipozungumza katika kipindi cha BBC Swahili.

Mbunge huyo aliyepigwa risasi mjini Dodoma yapata mwaka mmoja uliopita amesema katika kipindi cha miaka miwili ya sasa, upinzani umeshambuliwa kwa kiwango kikubwa.

Alisema hivyo baada ya kuulizwa swali na mtangazaji Zuhura Yunus kwamba, upinzani umelegalega nchini Tanzania.

Alijibu swali hilo Lissu amesema, itakua ajabu kama upinzani utabaki vile katika kipindi hiki.

“Wapinzania hawajanyamaza, ila umeshambuliwa,” amesema Lissu na kuongeza “ni ajabu kama tungeendelea kuwa kama wa Kikwete (Rais Kikwete, Rais Mkapa).

Pia Lissu amesema kuwa, Bunge lilitoa taarifa ya kukataa kumlipia matibabu kwa madai ya kutofuata utaratibu.

Amesema, atapona vizuri atarejea nchini huku akiwa na tahadhari.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaTangulizi

Ngoma bado mbichi mkataba wa Bandari

Spread the love  SAKATA la mkataba wa uendeshaji, uendelezaji na uboreshaji wa...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mkataba unaweza kuvunjwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

BiasharaTangulizi

Mkurugenzi TPA: Mikataba ya utekelezaji bado haijasainiwa

Spread the loveMKURUGENZI Mkuu wa Mamlaka ya Usimamizi wa Bandari Tanzania (TPA),...

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

error: Content is protected !!