MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Chadema Bara, Tundu Lissu, amesema mchakato wa upatikanaji katiba mpya ni mgumu, kwani unachukua muda mrefu na kushauri uanze mara moja. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Lissu ametoa kauli hiyo leo Jumatano, tarehe 9 Machi 2022, akihutubia kupitia mtandao wa kijamii wa ClubHouse, akiwa nchini Ubelgiji.
Makamu Mwenyekiti huyo wa Chadema, amesema hata mchakato wa upatikanaji katiba mpya nchini Kenya, nao ulichukua muda mrefu, kwa kuwa ulianza 1998 hadi 2010, ilipoatikana.
“Kwa hiyo mchakato ni mgumu na kama mtu anaamini kwamba tunaweza tukaipata ndani ya mwaka mmoja Mungu amsaidie. Hatuwezi kuipata ndani ya mwaka mmoja, miwili, mitatu, minne au mitano.Lazima tuanze mchakato,” amesema Lissu.
Lissu amesema, muda wa kukamilika kwa mchakato huo utategemea na watu watakaoshiriki zoezi hilo.
“Urefu wa hiyo njia itaamriwa na hao watakaosafiri hiyo njia, tukisafiri kwa pamoja, kwa kukubalina na mambo ya msingi, njia itakuwa fupi. Tukiiafiri kwa kuvuta, kutoboana macho, kupigana na kufungana njia itakuwa ndefu zaidi,” amesema Lissu.
Mwanasiasa huyo amesema, kama mchakato wa upatikanaji katiba mpya hautakamilika ifikapo 2025, kuna uwezekano wa kufanya marekebisho madogo ya katiba kwa ajili ya Uchaguzi Mkuu, huku ukiendelea.
Mchakato wa upatikanaji katiba mpya ulianza rasmi nchini Tanzania 2011, kwa utungwaji wa Sheria ya Mabadiliko ya Katiba Na. 83/2011, kisha ikatungwa Sheria ya Kura ya Maoni Na. 11/2013.
Mchakato huo uliendelea hadi 2015, ulipokwama katika hatua ya kura za maoni za kupitisha katiba pendekezwa, kutokana na zoezi la uandikishaji wapiga kura lililokuwa linafanywa na Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC), kutokamilika.
Asante ndugu lissu nakupongeza kwa kutimzmiza wajibu moja ya kazi ya kiongozi ni kuongea and kuonesha vitendo ambavyo wananchi wataviiga sasa lissu ukiwa kama kiongozi unawo waongoza waige nini kutoka kwa kwo