Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu alia kutelekezwa
Habari za Siasa

Lissu alia kutelekezwa

Tundu Lissu
Spread the love

TUNDU Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amelalamika kutelekezwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Akizungumza na kwenye mkutano wa hadhara jijini humo tarehe 17 Oktoba 2020, Lissu amesema tofauti na mikoa mingine aliyokwenda kufanya kampeni, katika jiji hilo hawakupata msaada wowote kutoka kwa polisi.

Ametumia jukwa la kisiasa kumfikishia ujumbe Mkuu wa Jeshi la Polisi chini (IGP), Simon Sirro kwamba, Polisi Dodoma kuna tatizo.

“Katika Makao Makuu ya nchi yetu, tumeachwa hivi hivi na Jeshi la Polisi la mkoa huu, tunajihangaikia wenyewe barabarani.

Tundu Lissu, Mgombea Urais wa Tanzania kwa tiketi ya Chadema akivuka Ziwa Victoria kwa kutumia kutumia mtumbwi akieleka Ukelewe

“Yaani IGP (Simon Sirro) kama unanisikia, huna RPC (mkuu wa jeshi la polisi wa mkoa) hapa…., inakuwaje mgombea urais yeye ndiye anayeongoza msafara kwenye malori makubwa kama haya?

“Ni utendaji gani huu? Tumesindikizwa kila mahali na polisi isipokuwa hapa Makao Makuu ya nchi,” amesema.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mbunge ataka kasi uzalishaji walimu ipunguzwe akidai hakuna ajira

Spread the loveMBUNGE wa Mlalo (CCM), Rashid Shangazi, ameishauri Serikali ipunguze kasi...

error: Content is protected !!