TUNDU Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amelalamika kutelekezwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Dodoma. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).
Akizungumza na kwenye mkutano wa hadhara jijini humo tarehe 17 Oktoba 2020, Lissu amesema tofauti na mikoa mingine aliyokwenda kufanya kampeni, katika jiji hilo hawakupata msaada wowote kutoka kwa polisi.
Ametumia jukwa la kisiasa kumfikishia ujumbe Mkuu wa Jeshi la Polisi chini (IGP), Simon Sirro kwamba, Polisi Dodoma kuna tatizo.
“Katika Makao Makuu ya nchi yetu, tumeachwa hivi hivi na Jeshi la Polisi la mkoa huu, tunajihangaikia wenyewe barabarani.
“Yaani IGP (Simon Sirro) kama unanisikia, huna RPC (mkuu wa jeshi la polisi wa mkoa) hapa…., inakuwaje mgombea urais yeye ndiye anayeongoza msafara kwenye malori makubwa kama haya?
“Ni utendaji gani huu? Tumesindikizwa kila mahali na polisi isipokuwa hapa Makao Makuu ya nchi,” amesema.
Leave a comment