Saturday , 3 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu akumbana na kikwazo Chato
Habari za Siasa

Lissu akumbana na kikwazo Chato

Tundu Lissu
Spread the love

TUNDU Lissu, mgombea urais wa Tanzania kupitia Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), amekumbana na kituko cha kwanza Chato mkoani Geita. Anaripoti Mwandishi Wetu, Chato … (endelea).

Taarifa kutoka Chato zinaeleza, usiku wa kuamkia leo Jumanne tarehe 13 Oktoba 2020, eneo la biashara la Masai  Machae, mgombea ubunge kupitia chama hicho katika jimbo hilo, limevamiwa na kuvunjwa.

Lissu kwenye ukurasa wake wa twitter amesema, licha ya uvamizi na vitisho hivyo, mkutano wake wa kampeni aliopanga kuufanya leo, utatekelezwa bila hofu yoyote.

“Leo ni siku ya mkutano wetu Jimbo la Chato na tayari wameanza kutufanyia fujo. Usiku wa kuamkia leo wamevamia biashara ya Mgombea ubunge wetu na nyumba ya Katibu wa Jimbo na kuharibu mali zao. Hatutishiki na hatutatishika. Mkutano wetu wa Chato uko pale pale,” amesema Lissu.

Mgombea huyo ambaye pia ni makamu mwenyekiti wa Chadema, anamalizia kampeni zake katika Mkoa wa Shinyanga na leo atafanya kampeni majimbo ya Bukombe, Mbogwe na mkutano wa mwisho utakuwa Chato.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!