Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lissu aichokonoa ATCL, ashusha hoja zake
Habari za SiasaTangulizi

Lissu aichokonoa ATCL, ashusha hoja zake

ATCL Dreamliner
Spread the love

TUNDU Lissu, Mwanasheria Mkuu wa Chadema, amehoji faida halisi inayotokana na Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), tangu Rais John Magufuli aingie madarakani. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kupitia ukurasa wake wa Twitter leo tarehe 30 Oktoba 2019, Lissu amesema, kuna haja ya kuangalia upya uendeshaji hilo liingize faida.

“Hadi sasa Magufuli (Rais) kanunua ndege 7 sawa na matumizi ya Sh. 1.769 trilioni, na kuingiza Bil 30 tu kama faida ndani ya ATCL, kwa nini hatuoni kuna haja ya kuangalia namna ya kufanya biashara hii upya,” amedai Lissu.

https://twitter.com/tundu_lissu/status/1189586737611395073?s=21

Kwenye andishi hilo amehoji,  kwanini wataalamu wa masuala ya uchumi wameruhusu serikali kutumia Sh 1.7 Trilioni, kununua ndege katika kipindi cha miaka mitatu, wakati uwekezaji huo hautaleta faida mapema.

“Wachumi mnaruhusu vipi kutoa Tril 1.769 ndani ya miaka 3, zisizo kuwa na matarajio ya kurudi leo au kesho? ” amehoji Lissu.

Wakati huo huo, Lissu amehoji, ndege hizo zinanunuliwa kwa masilahi ya mtu mmoja au kwa ajili ya kufanya biashara? Na kueleza, fedha hizo zingesaidia kuboresha afya, elimu, miundombinu na kutoa ajira.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za SiasaTangulizi

Shibuda amlima waraka mzito Bulembo

Spread the loveMKONGWE wa siasa nchini, John Shibuda amemshukia kada maarufu wa...

error: Content is protected !!