TUNDU Lissu, Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Bara, nchini Tanzania, amefanyiwa upasuaji wa 25. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).
Ni mwendelezo wa matibabu anayoyapata tangu aliposhambuliwa kwa risasa zadi ya 30 huku 16 zikimpata mwilini, mchana wa tarehe 7 Septemba 2017, akiwa katika makazi yake Area D jijini Dodoma.
Alikutana na makasa huo, wakati akitoka kuhudhuria mkutano wa Bunge uliokuwa ukiendelea.
Today I underwent the 25th surgical op of the September 7, 2017, assassination attempt. With Magufuli gone, it's time new President Samia told me, the nation & the world who's behind the shooting & why? Who gave what order to whom? Her silence on this issue can't hold any longer! pic.twitter.com/pPeicwauuv
— Tundu Antiphas Lissu (@TunduALissu) June 8, 2021
Mara baada ya kushambuliwa, Lissu alipelekwa Hospitali ya Rufaa ya Dodoma kwa matibabu ya awali kisha, usiku wa siku hiyohiyo, alihamishiwa Hospitali ya Nairobi nchini Kenya.
Alipata matibabu Nairobi hadi tarehe 6 Januari 2018, alihamishiwa nchini Ubelgiji kwa ajili ya matibabu zaidi.
Jana Jumanne, tarehe 8 Juni 2021, Lissu alitumia ukurasa wake wa Twitter aliweka picha na kuandika “nimefanyiwa upasuaji wa 25.”
Tunakusaidiaje sasa kama ni 25