Saturday , 2 December 2023
Home Kitengo Michezo Ligi Kuu Bara kurejea Juni 13, 2020
Michezo

Ligi Kuu Bara kurejea Juni 13, 2020

Spread the love

MTENDAJI Mkuu wa Bodi ya Ligi, Almasi Kasongo ametangaza tarehe ya kurejea kwa michezo ya Ligi Kuu Tanzania Bara, ambayo ni Juni 13, huku ratiba kamili ikitarajiwa kupangwa Mei 31, 2020. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Kuendelea kwa michezo hiyo ni kufuatia agizo la Rais John Magufuli kutanga shughuli za michezo kuendelea kufuatia kuwepo kwa mwenendo mzuri wa mlipuko wa ugonjwa Corona nchini.

Taarifa ya kuendelea na michezo hiyo kutoka bodi ya Ligi imetolewa kwenye kurasa yao kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter baada ya kuwa na vikao vya muda mrefu na kusubiri muongozo kutoka Serikalini.

Baada ya agizo hilo baadhi ya klabu mbalimbali wa Ligi Kuu tayari zimeanza maandalizi ya kumalizia michezo iliyosalia ambayo itachezwa katika kituo kimoja Jijini Dae es Salaam kwenye Uwanja wa Taifa, Uhuru na Azam Complex.

Ligi hiyo ilisimama mwezi Machi kufuatia agizo la Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ya kutaka shughuli zote za michezo kusimama kutokana na mlipuko wa ugonjwa wa Covid-19, huku klabu ya Simba ikiwa vinara kwenye msimamo wakiwa na alama 72.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Fernandes hakamatiki Man Utd, mahesabu ni kuifunga Bayern

Spread the love  NAHODHA wa Manchester United, Bruno Fernandes, alikuwa na kiwango...

Michezo

Meridianbet na Ligi ya Europa inakupa pesa za kumwaga mapema sana

Spread the love  KOMBE la UEFA Europa League ni zito kuliko makombe...

Michezo

Kwapua mpunga na mechi za UEFA leo na kesho

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya kuendelea leo na kesho...

AfyaMichezo

GGML yatoa milioni 17 kung’arisha ATF Marathon

Spread the loveKATIKA kuendelea kuunga mkono jitihada za Serikali kukabiliana na maambukizi...

error: Content is protected !!