Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Michezo Namungo yafuzu makundi, yakubali kipigo bao 3-1
Michezo

Namungo yafuzu makundi, yakubali kipigo bao 3-1

Spread the love

 

LICHA ya kupoteza kwa mabao 3-1, kwenye mchezo wa mzunguko wa pili wa Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Costo De Agosto kutoka Angola, timu cha Namungo FC imefuzu hatua ya makundi ya michuano hiyo. Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Namungo FC imefanikiwa kufuzu kwenye hatua hiyo ya makundi kwa jumla ya mabao 7-5, mara baada ya kupata ushindi kwenye mchezo wa kwanza wa mabao 6-2, uliofanyika kwenye dimba la Azam Complex, Chamazi.

Katika mchezo huo wa leo uliofanyika pia kwenye dimba la Azam Complex, Chamazi, Costo De Agosto walikuwa wanajaribu kujiuliza kuona kama watafanikiwa kupata idadi kubwa ya mabao ili kuweza kufuzu kwa hatua inayofuata lakini mambo yalionekana kuwa magumu.

Kwa matokeo hayo Namungo itaangukia kundi D, sambamba na Raja Casablanca kutoka Morocco, Pyramids ya Misri pamoja na Nkana Red Devil kutoka Zambia.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMichezo

Mwana FA anogesha Tamasha la Exim Bima Festival

Spread the loveNAIBU Waziri Wa Utamaduni, Sanaa Na Michezo, Hamis Mwinjuma ‘Mwana...

Michezo

Manchester City dhidi ya Tottenham ni usiku wa kisasi

Spread the love KIPUTE kati ya klabu ya Manchester City dhidi yaTottenham Hotspurs...

Michezo

Wikiendi ya kutamba na Meridianbet hii hapa usikubali kuikosa

Spread the loveMERIDIANBET wanakwenda kukupa nafasi ya kutambawikiendi hii kupitia ODDS KUBWA walizoweka...

Michezo

Fernandes hakamatiki Man Utd, mahesabu ni kuifunga Bayern

Spread the love  NAHODHA wa Manchester United, Bruno Fernandes, alikuwa na kiwango...

error: Content is protected !!