Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Lema arusha dongo bungeni
Habari za SiasaTangulizi

Lema arusha dongo bungeni

Godbless Lema, Aliyekuwa Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema)
Spread the love

 

LICHA ya Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kuwa na wabunge kutoka upinzani, Godbless Lemba ambaye alikuwa Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), amesema Watanzania wameanza kukumbuka sauti ya wapinzani bungeni. Anaripoti Regina Mkonde, Dar es Salaam…(endelea).

Lema anayeishi uhamishoni nchini Canada baada ya kuondoka Tanzania kwa madai ya kuhofia usalama wake, ametoa kauli hiyo tarehe 5 Februari 2021, wakati akizungumzia utendaji wa Bunge la 12 linaloongozwa na Spika Job Ndugai.

Akizungumza kwenye mahojiano na chombo cha Habari cha mtandaoni, Lema amedai Bunge lililoanza hivi karibuni, halina ushawishi kwa wananchi kama mabunge yaliyopita, ambayo yalikuwa na wabunge wengi wa upinzani wa kuchaguliwa.

“Bunge leo umeliona halina hata wiki mbili wala halina mwezi, ndio kwanza limeanza juzi unaona mawazo ya umma kwamba wanaanza kujisikia kuna kitu wame-miss (wamekosa),” amesema Lema.

Katika Uchaguzi Mkuu uliofanyika tarehe 28 Oktoba 2020, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilipata viti zaidi ya 360 vya ubunge, huku vyama vya upinzani vikiambulia majimbo 6.

Chadema kilipata jimbo moja saw ana Chama cha Wananchi (CUF), Chama cha ACT-Wazalendo kilipata majimbo menne Zanzibar.

Wabunge wa kuchaguliwa wa CUF ni Shamsia Mtamba, Mtwara Vijijini na Chadema ni Aidah Khenan, Jimbo la Nkasi.

Wabunge wa ACT-Wazalendo ni Khatibu Saidi Haji (Konde), Salum Mohamed Shafi (Chonga), Omar Ali Omar (Wete) na Khalifa Mohamed Issa (Mtambwe).

bunge la tanzania

Kuhusu hatima yake ya kisiasa, Lema amewahakikishia Watanzania kwamba atarejea nchi ni ili kuendeleza mapambano ya demokrasia.

Amesema, demokrasia ya Tanzania haitaimarishwa kwa kufanyika uchaguzi, bali itaimarika kwa kutumia nguvu ya umma, na kwamba hivi karibuni Watanzania wataamua kuhusu hilo.

“Niseme tu kwamba sisi tuko nje ya mipaka, ilibidi tuwe nchini, niwahakikishieni kwamba tutaenda nyumbani wakati ambao muafaka na haiko mbali Watanzania wataamua,” amesema Lema.

Mwanasiasa huyo aliondoka Tanzania kwenda Nairobi nchini Kenya kisha Canada, mwishoni mwa mwaka jana baada ya matokeo ya uchaguzi mkuu wa 2020.

Lema alidai, kwamba ameamua kuondoka nchini kutokana na kupokea vitisho kutoka kwa watu wasiojulikana.

Hata hivyo, Mkuu wa Jeshi la Polisi Tanzania, IGP Simon Sirro alikanusha kuwepo kwa taarifa za vitisho kwa Lema, alimtaka wanasiasa wengine waliokimbilia nje ya nchi baada ya uchaguzi mkuu, kurudi nyumbani kwani kuna usalama wa kutosha.

1 Comment

  • Asante ndugu lema kama imeandikwa fungu la kukosa ni vigumu kufutwa acha hoja zisizo and msingi

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

TEMESA iliyokarabati Kivuko kwa Bil 7.5 yapata hati chafu

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

ACT-Wazalendo yakusanya Mil 8.5/- kodi ya zuio na kutokomea nazo

Spread the love  MDHIBITI na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG),...

Habari za Siasa

DC Kasilda Mgeni ahamasisha chakula shuleni

Spread the love  MKUU wa Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro, Kasilda Mgeni...

Habari za Siasa

Bilioni 223.9 zapelekwa Tunduru ndani ya miaka 2 ya SSH

Spread the love  ZAIDI ya Sh. bilioni 223.9 zimepelekwa Wilaya ya Tunduru...

error: Content is protected !!