Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lema apigwa, visu vyatamba Arusha
Habari za SiasaTangulizi

Lema apigwa, visu vyatamba Arusha

Spread the love

GODBLESS Lema Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema) ameshushiwa kipigo kutoka kwa walinzi wa Chama Cha Mapinduzi (CCM). Anaandika Mwandishi Maalum Arusha … (endelea).

Tayari taarifa ya kipigo hicho ameifikisha katika Jeshi la Polisi ambapo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha, Kamanda Ramadhani Ng’azi amethibitisha kupokea taarifa ya Lema kupigwa na walinzi wa CCM.

Wakati Lema akishambuliwa, Ibrahim Ismail ambaye ni wakala wa Chadema Kata ya Kaloleni mkoani humo ameripotiwa kushambuliwa kwa kuchomwa visu.

Mwingine aliyeshambuliwa kwenye tukio hilo na taarifa yake kumfikia Kamanda Ng’azi ni pamoja na Boniface Kimario, Mgombea Udiwani Kata ya Kaloleni pia Iddi Mukuru, Mwenyekiti wa CCM Kata ya Kaloleni anayedaiwa kujeruhiwa kwa kuchomwa visu na wafuasi wa Chadema.

Chadema ni miongoni mwa vyama vinavyoshiriki uchaguzi mdogo unaofanyika leo Jumapili katika maeneo mbalimbali Tanzania Bara.

Kufuatia vurugu hizo, Kamanda Ng’azi amesema polisi imefungua jalada la uchunguzi pamoja na kuanzisha msako wa kuwabaini waliohusika na vurugu hizo.

Amesema majeruhi walipelekwa katika Hospitali ya Mkoa ya Mount Meru ili kupatiwa matibabu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!