Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Lema apata hifadhi ya ukimbizi Canada
Habari za SiasaTangulizi

Lema apata hifadhi ya ukimbizi Canada

Godbless Lema
Spread the love

ALIYEKUWA Mbunge wa Arusha Mjini (Chadema), Godbless Lema amepata hifadhi ya ukimbizi ya kisiasa nchini Canada. Anaripoti Mwandishi Wetu, Nairobi … (endelea).

Lema aliyekuwa mbunge wa Arusha Mjini kati ya mwaka 2010-2020, ameondoka jana Jumatano tarehe 9 Desemba 2020 kwenda Canada yeye pamoja na familia yake akitokea jijini Nairobi nchini Kenya.

Lema alikuwa Kenya tangu tarehe 8 Novemba 2020 alipokwenda nchini humo kwa lengo la usalama wake baada ya kumalizika kwa Uchaguzi Mkuu uliofanyika 28 Oktoba 2020, yeye akiwa mgombea wa Arusha Mjini.

Hata hivyo, Lema alishindwa kwenye uchaguzi huo na Mrisho Gambo wa Chama tawala- Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Godbless Lema akiwa na watoto wake

Mara baada ya kuingia Kenya, alikamatwa kwa kile kilichoelezwa ni kuingia pasina kufuata taratibu. Hata hivyo, aliachiwa ili kuendelea na taratibu za kutafuta hifadhi ya kisiasa.

Picha mbalimbali zimemwonyesha Lema akiwa na familia yake (mke wake , Neema na watoto wake watatu) pamoja na Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe muda mfupi kabla ya kuondoka Kenya kwenda Canada.

Katika ukurasa wake wa facebook, Lema ameweka picha hizo na kuandika ‘We shall meet again’ akiwa na maana ‘tutaonana baadaye.’

1 Comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Mavunde aagiza Perseus kuharakisha fidia Sengerema

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameipongeza Kampuni ya Perseus kwa...

Habari za Siasa

Kigogo Chadema awanyooshea vidole vigogo serikalini kuhusu ripoti ya CAG

Spread the love  MJUMBE wa Kamati Kuu ya Chama cha Demokrasia na...

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

error: Content is protected !!