Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko LATRA yatangaza nauli mpya, daladala, mikoani
Habari MchanganyikoTangulizi

LATRA yatangaza nauli mpya, daladala, mikoani

Spread the love

MAMLAKA ya Udhibiti wa Usafiri Ardhini (LATRA) imetangaza viwango vya nauli mpya za daladala na mabasi ya kwenda mikoani. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Viwango hivyo vimetangazwa leo Jumamosi Tarehe 30, 2022 na Mkurugenzi Mkuu wa LATRA, Gilliard Ngewe, wakati akizungumza na waandishi wa Habari.

Ngewe amesema viwango vipya vya nauli vitaanza kutumika baada ya siku 14.

Kwa nauli za mikoani amesema mabasi ya daraja la kawaida kwa kwa kilometa 1 imeongezeka kutoka Sh. 36 kwa kilometa moja hadi Sh. 41.

Kwa daraja la kati imeongezeka kutoka Sh. 53 kwa kilometa moja hadi Sh56.88.

Ameongeza kuwa kwa mabasi ya mjini kuanzia kilomita 0 hadi 10 nauli itakuwa Sh. 500 badala ya Sh. 400 na nauli ya Sh. 450 itakuwa Sh. 550.

Amesema kuwa kwa kilomita 30 nauli itakuwa Sh. 850 badala ya Sh. 750 na kwa kilometa 35 nauli itakuwa Sh. 1000 huku kilometa 40 ikiwa ni Sh.1100.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

error: Content is protected !!