Kiungo wa kati wa zamani wa klabu ya Chelsea Frank Lampard, ameteuliwa kuwa kocha mpya wa klabu ya Everton kwa mkataba wa miaka miwili na nusu. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)
Lampard amejiunga na Everton akichukua mikoba ya Rafael Benited aliyetimuliwa kwenye kikosi hiko kufuatia kupata matokeo mabaya kwenye michezo ya Ligi Kuu msimu huu 2021/22.
Katika michezo 13 aliyocheza akiwa na Everton Benitez ameshinda mechi moja tu, na kuifanya timu hiyo kushika nafasi ya …. Kwenye msimamo wa Ligi.
Kibarua cha kwanza cha Lampard kitakuwa siku ya jumamosi katika mchezo wa mzunguko wane wa kombe la FA, dhidi ya Brentford kwenye dimba la Goodison Park.
Hiki kinakuwa kibarua cha kwanza cha Lampard, tangu alipofurushwa ndani ya klabu ya Chelsea kama kocha mkuu na nafasi yake kuchukuliwa na Thomas Tuchel.
Leave a comment