Tuesday , 5 December 2023
Home Kitengo Michezo Lampard astaafu soka
Michezo

Lampard astaafu soka

Frank Lampard
Spread the love

KIUNGO wa zamani wa klabu ya Chelsea, New York City FC na timu ya taifa ya England, Frank Lampard (38) leo ametangaza kustaafu mchezo wa mpira wa miguu baada ya kuucheza kwa mafanikio katika kipindi cha miaka 21, anaandika Kelvin Mwaipungu.

Lampard ambaye mpaka anatangaza kustaafu soka ameshinda mataji matatu ya Ligi Kuu England, mataji mawili ya Kombe la Ligi, mataji matatu ya kombe la chama cha soka nchini England (FA) na taji la Klabu Bingwa Ulaya mara moja.

Mkongwe huyo ametangaza uamuzi wake wa kustaafu soka kupitia kwenye ukurasa wake unaopatikana kwenye mtandao wa kijamii wa Instagram baada ya kuandika waraka mrefu kwenda kwa washabiki zake na wapenzi wa soka wote ulimwenguni.

Lampard aliandika kuwa huu ndio wakati sahihi wa yeye kustaafu mpira licha ya kupokea ofa nyingi ili aendelee kucheza mpira.

“Baada ya miaka 21 ya kucheza mchezo wa soka, sasa nimeamua kwamba ni wajati muafaka wa kustaafu mpira kama mchezaji wa kulipwa.”

“Wakati huo nimepokea ofa nyingi na nzuri kutoka nyumbani na nje ya nchi ili niendelee kucheza mpira, lakini kwa umri huu wa miaka 38 najisikia sasa ni wakati wa kuanza sura mpya katika maisha yangu,” aliandika Lampard kwenye ukurasa wake wa Instagram.

Mpanga anatangaza kutundika daruga, Lampard amecheza jumla ya michezo 106 katika timu ya taifa, na kuweka rekodi ya kuwa mfungaji bora wa muda wote wa klabu ya Chelsea baada ya kufunga mabao 211 kwa mashindano yote aliocheza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaMichezo

Mwana FA anogesha Tamasha la Exim Bima Festival

Spread the loveNAIBU Waziri Wa Utamaduni, Sanaa Na Michezo, Hamis Mwinjuma ‘Mwana...

Michezo

Manchester City dhidi ya Tottenham ni usiku wa kisasi

Spread the love KIPUTE kati ya klabu ya Manchester City dhidi yaTottenham Hotspurs...

Michezo

Wikiendi ya kutamba na Meridianbet hii hapa usikubali kuikosa

Spread the loveMERIDIANBET wanakwenda kukupa nafasi ya kutambawikiendi hii kupitia ODDS KUBWA walizoweka...

Michezo

Fernandes hakamatiki Man Utd, mahesabu ni kuifunga Bayern

Spread the love  NAHODHA wa Manchester United, Bruno Fernandes, alikuwa na kiwango...

error: Content is protected !!