Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Maisha Elimu La sita, la tano wasoma chumba kimoja
Elimu

La sita, la tano wasoma chumba kimoja

George Simbachawene, Waziri wa Ofisi ya Rais,Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa
Spread the love

WANAFUNZI wa shule ya msingi Magwalisi wilayani Mbarali mkoani Mbeya, wanatumia chumba kimoja, kwa wakati mmoja wakati wa kufundishwa wanafunzi wa madarasa wa ngazi tofauti kutokana na uchache wa vyumba vya madarasa, anaandika Esther Macha.

Jonathan Chengula, Mwalimu Mkuu wa shule hiyo amesema kuwa shule yao ina vyumba vinne tu vya madarasa, hali ambayo inawapa ugumu wakati wa ufundishaji wa wanafunzi.

“Tungeweza kuchangiwa na wazazi tukaongeza madarasa hata hivyo, shule ipo kwenye mgogo na inadaiwa kuwa ndani ya mipaka ya Mamlaka ya Hifadi ya Taifa (TANAPA), hivyo wazazi wanahofia kuongeza vyumba vya madarasa kisha shule ije kuhamishwa,” amesema Chengula.

Wema Amosi, mwanafunzi wa darasa la saba katika shule hiyo, amesema; “Tunaiomba serikali ituongezee majengo mengine ili tuweze kumudu masomo ambayo tunafundishwa darasani, tukiongezewa vyumba vya madarasa itakuwa msaada mkubwa kwetu.”

Clemencia Kitalima, mwanafunzi mwingine wa darasa la sita, amesema uchache wa vyumba vya madarasa umekuwa ukipelekea chumba kimoja kusomea wanafunzi wa madarasa mawili hali ambayo inaawathiri wanafunzi hao kutokana na kutosoma kwa nafasi.

“Tunaingia chumba kimoja ingawa sisi ni madarasa mawili tofauti kwahiyo tunageuziana migongo na walimu wawili tofauti wanatufundisha,” amesema.

Goden  Mgombavanu, mwenyekiti wa kitongoji cha Nyalunga, ilipo shule hiyo amemwambia mwandishi wa habari hii kuwa, changamoto kubwa iliyopo ni mgogoro wa mipaka ya Tanapa,  hivyo kushindwa kuendelea na ujenzi kwa hofu ya kuja kuhamishwa.

“Ni kweli, shule hii ina vyumba vichache na watoto wetu wanateseka hivyo ni vema serikali ikaliona hili ili mipaka halisi ya shule uweze kufahamika na wazazi waweze kuendelea na ujenzi wa vyumba vya madarasa kwa gharama zao,” amesema Mgombavanu.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaElimu

NMB yatoa vifaa vya ujenzi kwa shule sita Nyasa  

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa msaada wa vifaa mbalimbali vya ujenzi...

ElimuHabari Mchanganyiko

GGML yawapa mbinu wanafunzi Geita Boys kufikia malengo ya kitaaluma

Spread the loveKampuni ya Geita Gold Mining Limited (GGML) imetoa mafunzo maalumu...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanawake GGML wawanoa wanafunzi Kalangalala Sec. kujitambua

Spread the loveKATIKA kuadhimisha Siku ya Kimataifa ya Wanawake Duniani, Umoja wa...

ElimuHabari Mchanganyiko

RC Songwe ang’aka kesi 2 kati ya 60 za mafataki kuamuliwa

Spread the loveMkuu wa mkoa wa Songwe Dk. Fransis Michael ameshangazwa na...

error: Content is protected !!