Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kwanini CUF imeshindwa kesi ya kugombania majengo na ACT-Wazalendo
Habari za Siasa

Kwanini CUF imeshindwa kesi ya kugombania majengo na ACT-Wazalendo

Ado Shaibu, Katibu Mkuu wa ACT-Wazalendo
Spread the love

 

MAHAKAMA Kuu Zanzibar Masjala ya Tunguu imesema kuwa Chama cha Wananchi CUF hakina ushahidi wa kutosha wa kuithibitishia mahakama hiyo kuwa majengo ya Chama cha ACT-Wazalendo ni yao. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Hukumu hiyo imetolewa Jumatano tarehe 11 Janauri, 2023 na Jaji George Kazi baada ya kusikiliza kwa miaka mitatu shauri hilo namba 16 ya Mwaka 2019 kwa miaka mitatu .

Shauri hilo lilifunguliwa na Bodi ya wanadhamini ya Chama cha Wananchi CUF, wakiwalalamikia wanachama 19 wa ACT akiwemo Kiongozi wa Chama hicho Zitto Kabwe.

Walalamikiwa wengine kwenye shauri hilo ni pamoja na Salim Bimani, Joran Bashange, Ismail Jussa, Nassoro Mazrui, Thubeit Khamis Faki, Saleh Nassor Juma, Awadh Ali Said, Ali Abdallah, Zahra Ali Hamad, Raisa Abdallah Mussa, Fat’hiya Zahran, Said Ali Mbarouk, Riziki Omar Juma, Mohamed Juma Khatib, Tahir Awezi Mohamed. Khatib Hamad Shehe, Ali Abeid, Juma Abdulla Khatib, na Chama cha ACT Wazalendo.

CUF ililalamika kuporwa majengo ya Chama hicho pamoja na lile la Vuga, Mtendeni Ofisi ya Kilima Hewa, Mfenesini, Ofisi ya CUF ya Wilaya ya Micheweni iliyokuwepo Majenzini, Ofisi ya Koani iliyokuwa kwenye sheha ya Changaweni, Chumani, Nungwi Kaskazini ‘A’, Mkototoni, Ofisi ya Chakechake, sambamba na matawi kadhaa huku visiwani Zanzibar.

Jaji Kazi kwenye hukumu yake ameeleza kuwa CUF haikuwa na nyaraka zitakazoweza kuithibitishia mahakama hiyo kuwa majengo hayo ni halali yao.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!