Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Kuziona Simba, Yanga Sh. 7,000
Michezo

Kuziona Simba, Yanga Sh. 7,000

Spread the love

SHIRIKISHO la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF) leo limetangaza viingilio vya mchezo wa Ligi Kuu unaowakutanisha watani wa jadi Yanga na Simba utakaochezwa kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam, ambapo kiingilio cha chini kitakuwa ni Sh. 7,000. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea)

Viingilio vingine katika mchezo huo unaotarajiwa kuchezwa Jumamosi 16 Ffebruari, 2019 vitakuwa ni Sh. 30,000 kwa VIP A na 20,000 kwa VIP B na C.

Kuelekea mchezo huo Yanga inatarajia kuweka kambi mkoani Morogoro wakitokea Tanga, huku Simba wakisalia Dar es Salaam ambapo wanajiandaa na mchezo wao wa Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Al Ahly unaotarajiwa kuchezwa 12 Februari, 2019.

Yanga inaingia kwenye mchezo huo ikiwa kileleni kwenye msimamo wa ligi kwa kukusanya jumla ya pointi 58 baada ya kucheza michezo 23, huku Simba ikiwa kwenye nafasi ya tatu na kukusanya pointi 36 baada ya kucheza michezo 15.

Mara ya mwisho timu hizi kukutana ilikuwa kwenye mchezo wa Ligi Kuu Tanzania Bara 30 Septemba, 2018 na kumalizika kwa suluhu na kila timu ilifanikiwa kuondoka na alama moja.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!