Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Kuuza na kununua kemikali mpaka cheti
Habari Mchanganyiko

Kuuza na kununua kemikali mpaka cheti

Mkemia Mkuu wa Serikali Prof. Samwel Manyele
Spread the love

MKEMIA Mkuu wa Serikali Prof. Samwel Manyele ameagiza kuwa kila mtu atakayeuziwa au kununua kemikali lazima aoneshe cheti cha usajili kwa kuwa sheria inaagiza kila anayehusika na kemi kali ni lazima asajiliwe. Anaripoti Dany Tibason … (endelea).

Mbali na hilo amesema tangu kutungwa kwa Sheria ya usimamizi na udhibiti wa kemikali za viwandani na majumbani mwaka 2003, taasisi zaidi ya 3,000 zimesajiliwa na Mkemia Mkuu wa serikali.

Prof. Manyele ametoa kauli hiyo alipokuwa akifungua mafunzo ya wauzaji, wasafirishaji, wahifadhi na watumiaji wa kemikali katika kanda ya kati Dodoma.

Amesema anayeleta athari ni mtumiaji wa kemikali ni yule asiyefuata taratibu na kuwa chanzo cha madhara kwa wananchi.

“Wafanyabiashara mnaotumia kemikali mmeingia kwenye ‘level’ ya juu, tuwaombe sana hizo shughuli zenu msije mkathamini biashara zenu mkasahau afya ya watanzania na mazingira yetu ni kosa kisheria,” amesema Prof. Manyele.

Hata hivyo amesema adhabu itatolewa kwa kuzingatia kiwango cha mtaji wa biashara yako.

“Niwaombe sana muwe mnazingatia hii sheria kwa kuwa kemikali nyingi zilikuwa zinaingia nchini kiholela na watumiaji wengi walikuwa wanaingiza kiholela,” amesema Mkemia huyo.

Amesema kuwa serikali inasisitiza kufuata sheria bila shuruti na kufuata taratibu zilizoainishwa kisheria.

“Wapo watu ambao shughuli zao za siku nyingi na hawajapata usajili, lakini wote mtapata usajili uliosawa, niwaombe usimamizi na utekelezaji wa sheria unapaswa uzingatiwe sana,” amesema.

Amebainisha kuwa unaposajili kampuni wale watakaosimamia shughuli wawe waajiriwa na ikiwezekana ofisi ya Mkemia ione barua zao za ajira.

“Udhibiti kwasasa ni wa kiwango cha juu tangu sheria hii ianze kutumika ndani ya miaka 13 ambapo tumeweka mifumo ya udhibiti,” amesema.

Hata hivyo amesema wale wanaoingiza kutoka nje ya nchi udhibiti ni kubwa sana hivyo wajipange vizuri kwenye maeneo yote kwa kuwa atahakikisha anasimamia shughuli za kemikali kikamilifu.

“Serikali ina uwezo wa kutambua aina za kemikali na kiwango cha kemikali zinazoingia na zinaenda wapi, serikali inaendelea kuongeza kasi katika kuzuia matumizi yasiyo sahihi ya kemikali,” amesema.

Akizungumzia kuhusu mafunzo hayo, Mkemia huyo amesema ni muhimu kwa kuwa mbinu za matumizi ya kemikali zinabadilika hivyo ni vyema kupata mafunzo mara kwa mara.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!