Saturday , 20 April 2024
Home Kitengo Maisha Afya Kupima corona sasa Sh. 275,000
Afya

Kupima corona sasa Sh. 275,000

Spread the love

HOSPITALI ya Aga Khan imepewa jukumu la kupima virusi vya corona (COVID-19) kwa gharama ya Sh. 275,000 kwa Mtanzania. Anaandika Hamis Mguta, Dar es Salaam…(endelea).

Kwa wageni kutoka nje ya nchi, watatakiwa kulipa Sh. 360,000 ili kupata huduma hiyo.

Taarifa ya hospitali hiyo iliyotolewa leo tarehe 7 Januari 2021, imeeleza kupewa mamlaka hayo na Maabara ya Taifa.

Pia hospitali hiyo imepewa mamlaka ya kutoa cheti cha corona kwa niaba ya Wizara ya Afya.

“Kliniki itafunguliwa kuanzia saa 2:15 asubuhi mpaka saa 6:30 mchana (Jumatatu-Ijumaa) na saa 2:15 mpaka saa 5:30 asubuhi siku ya Jumamosi,” imeandika taarifa hiyo na kwamba, utaratibu huo utaanza tarehe 8 Januari 2021.

1 Comment

  • Je mvuja jasho atamudu kulipa sh 275,000? Yaani anayesafiri kutoka Tanga kwa basi hadi Mombasa nauli sh 10,000 halafu kupima korona sh 275,000?? Are we serious?
    Kwa nini kazi hiyo ipewe hospitali ya binafsi tena ya matajiri? Serikali haina hospitali na wataalamu wanaoweza kazi hiyo kwa bei nafuu?

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

AfyaHabari za Siasa

Serikali yasaka watumishi afya ngazi ya jamii 8,900

Spread the loveSERIKALI imeanza utekelezaji wa mpango jumuishi wa wahudumu wa afya...

AfyaHabari za SiasaTangulizi

Bima ya afya kwa wote kuanza Aprili, wajane kicheko

Spread the loveSHERIA ya Bima ya Afya kwa Wote, inatarajiwa kuanza kutumika...

AfyaHabari Mchanganyiko

Marekani kuipa Tanzania bilioni 980 kudhibiti VVU, UKIMWI

Spread the loveSERIKALI ya Tanzania inatarajiwa kupewa msaada wa fedha kiasi cha...

AfyaHabari Mchanganyiko

Wanavijiji wajenga zahanati kukwepa umbali mrefu kupata huduma

Spread the loveWANAVIJIJI wa Kata ya  Musanja Jimbo la Musoma Vijijini, mkoani...

error: Content is protected !!