Thursday , 28 March 2024
Home Kitengo Michezo Kundi la kifo lapoteana Euro
MichezoTangulizi

Kundi la kifo lapoteana Euro

Spread the love

 

HATUA ya 16 ya michuano ya Euro imemalizika jana, kwa kigogo mwengine wa soka barani humo, timu ya Taifa ya Ujerumani kutupwa nje mara baada ya kukubali kichapo cha mabao 2-0, kutoka kwa Uingereza. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea)

Kichapo hicho cha Ujerumani, kilikamilisha idadi ya timu kwenye kundi F, kuondolewa kwenye michuano hiyo, licha ya kuwa kundi gumu ‘Kundi la Kifo’ na kuwepo kwa matumaini mengi ya kuwa bingwa angetoka humo.

Kundi hilo lilikuwa na timu za Ureno ambao ni mabingwa watetezi, Timu ya Taifa ya Ufaransa ambao ni mabingwa wa kombe la Dunia, Ujerman pamoja na Hungary.

Katika kundi hilo zilipita timu tatu, kwenye hatua ya 16 bora, ambazo ni Ureno, Ufaransa ambao walikuwa vinara pamoja na Ujerumani iliyoshika nafasi ya pili.

Kwenye michezo hiyo ya hatua ya 16 bora, Ureno ilicheza dhidi ya Ubeligiji na kuondoshwa kwenye michuano hiyo mara baada ya kukubali kichapo cha bao 1-0, Ufaransa nao wakakubali kipigo kwa njia ya penati 5-4, dhidi ya Uswizi, mara baada ya kufungana mabao 3-3, kwenye dakika 90.

Ujerumani ilikuwa wa mwisho kwenye kundi hili kuaga mashindano siku ya jana, kwa kukubali kichapo cha mabao 2-0, kutoka kwa Uingereza, mabao yaliyofungwa na Raheem Sterling pamoja na Harry Kane.

Michuano hiyo itaendelea Ijumaa na juma mosi kwa hatua ya robo fainali ambapo Hispania itashuka dimbani dhidi ya Uswizi, Ubeligiji dhidi ya Italy, Jamhuri ya Czech wataminyana na Denmark, na Ukrain watavaana na timu ya Taifa ya Uingereza.

 

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

Habari za SiasaTangulizi

CAG aibua madudu halmashauri 10, TANESCO na MSD

Spread the loveRIPOTI ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali...

error: Content is protected !!