Saturday , 3 June 2023
Home Kitengo Michezo Kuiona Yanga vs Pyramids FC Sh. 10,000/=
Michezo

Kuiona Yanga vs Pyramids FC Sh. 10,000/=

Frederick Mwakalebela, Makamu Mwenyekiti wa Yanga
Spread the love

KLABU ya Yanga leo imetangaza rasmi kiingilio kwenye mchezo wa Klabu Bingwa Afrika dhidi ya Pyramids FC ya Misri utakaochezwa kwenye Uwanja wa CCM, Kirumba jijini Mwanza, ambapo kiingilio cha chini kitakuwa Sh. 10,000 na cha juu Sh. 70,000. Anaripoti Kelvin Mwaipungu… (endelea).

Makamu Mwenyekiti wa klabu hiyo, Frederick Mwakalebela amesema kuwa sababu ya kuweka kiingilio hicho ni kutokana na udogo wa kiwanja ambacho kinaingiza mashabiki wachache ukilinganisha na uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam.

“Tumeweka kiingilio cha Sh. 10,000 kwa sababu mapato yatakayopatikana yatakuwa na mgao mkubwa ambapo baadhi ya asilimia zitakwenda TFF, CAF, TRA na gharama za mchezo na ukizingatia uwanja ni mdogo na hivyo Yanga inaweza kukosa mapato,” alisema Mwakalebela.

Aidha kiongozi huyo aliongezea kuwa timu itaondoka kesho kuelekea Mwanza ambapo tarehe 22 itacheza mchezo wa Ligi Kuu dhidi ya Mbao FC na siku nne baadaye watacheza mchezo wao dhidi ya Pyramids kwenye uwanja huo huo.

Yanga itawakosa nyota wake watano kuelekea mchezo huo ambao ni Mohammed Issa na Issa Bigirimana wote hawa ni majeruhi, huku David Molinga na Mustapha Suleiman watakaa nje kutokana na kukosa vibali na beki kisiki Lamine Moro atakuwa anatumikia kadi nyekundu aliyoipata kwenye mchezo dhidi ya Zesco FC.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Dk. Mkwizu: Afrika tudumishe utamaduni

Spread the love  MWENYEKITI wa Jumuiya ya Tawala za Mitaa Mkoa wa...

Michezo

‘EONII’ kuteka tasnia ya filamu

Spread the love  UZINDUZI wa Filamu ya Kisayansi ya ‘EONII’ uliofanyika Mei...

Michezo

NBC Dodoma Marathon yazinduliwa, wakiambiaji 6,000 kushiriki

Spread the loveBENKI ya NBC imetangaza kufanyika kwa mbio kubwa za NBC...

Michezo

Rais Samia anunua tiketi 5000 Yanga vs USM Alger

Spread the loveRAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu...

error: Content is protected !!