Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea, Paresso, wanamtumia Lissu kuomba kura
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea, Paresso, wanamtumia Lissu kuomba kura

Spread the love

WaBUNGE wa Chadema – Saed Kubenea (Ubungo) na Cecilia Paresso (Viti Maalum), mkoani Arusha – wamemtumia mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, kumuombea kura mgombea udiwani wa kata ya Baray, wilayani Karatu, mkoani Arusha. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tukio hilo lilitokea leo jioni wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Qangded, kilichopo katika hiyo.

Akizungumza katika mkutano huo, Kubenea alimuomba Lissu ambaye wakati huo kuongea na wananchi wa kata hiyo ambayo ilikuwa inaongozwa na marehemu Thomas Moshi Darado. Lissu alikubali ombi hilo.

“…hapa nilipo niko na shujaa wa taifa hili, Mheshimiwa Tundu Lissu, ambaye nyote mnajua kilichompata. Yuko kwenye matibabu nje ya nchi. Anaomba kuzungumza na ninyi,” alisema Kubenea huku akishangiliwa na wananchi.

Naye Lissu akihutubia mkutano huo kwa njia ya simu aliwataka wananchi wa Qangded, kumchagua mgombea wa Chadema, Dagharo Hamay Kisimbi kwa maelezo kuwa ndiye mwenye sifa ya kufuata nyayo za diwani aliyekuwapo.

Alisema, “ndugu zangu wa kata ya Baray, mimi naitwa Tundu Lissu. Ninaongea kutoka nchini Ubelgiji ambako nimekuja kutibiwa. Kama ningekuwa na afya nzuri, basi leo ningekuwa nanyi hapo Baray.

“Mnajua kuwa marehemu  Tomas Darabe alikuwa rafiki yangu mkubwa. Hivyo basi, kwa heshima yake na heshima yangu kwenu, nawaomba sana mumchague diwani wa Chadema, ” alieleza.

Alisema, “katu wananchi wa Karatu, msikubali kurudishwa utumwani na CCM. Msikubali. Ninawaomba muendelee kutuunga mkono ili tuweze kuwahudumia.”

Kwa upande wake Kubenea alirejea kauli yake kuwa hana mapngo wa kuondoka Chadema na kuongeza kuwa wanaoeneza habari hiyo, “wanapaswa kupuuzwa.”

Alisema, “ndugu zangu nchi hii imejaa uonevu na njia pekee iliyosalia ya kuondoa uonevu huo na unyanyasaji, ni kukiondoa  Chama Cha Mapinduzi, madarakani.

“Nasikia watu wanasema nataka kujiunga na CCM. mimi siyo mtu wa kutanganga na wala siwezi kujiunga na chama kinachohubiri amani, lakini kikiwa kinatenda uhalifu.”

Aliwataka wananchi kumuenzi marehemu Darabe kwa kumchagua diwani  anayetokana na chama chake na ambaye kweli atakuwa mwakilishi wa wananchi.

Alisema, madai kuwa Chadema itashinda uchaguzi huo, lakini CCM ndio watakaotangazwa mshindi, hayana nafasi katika kata hiyo; yeye binafsi atakuwapo Karatu siku ya uchaguzi kuhakikisha mgombea wao anatangazwa mshindi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

error: Content is protected !!