Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea, Paresso, wanamtumia Lissu kuomba kura
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea, Paresso, wanamtumia Lissu kuomba kura

Spread the love

WaBUNGE wa Chadema – Saed Kubenea (Ubungo) na Cecilia Paresso (Viti Maalum), mkoani Arusha – wamemtumia mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu, kumuombea kura mgombea udiwani wa kata ya Baray, wilayani Karatu, mkoani Arusha. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Tukio hilo lilitokea leo jioni wakati wa mkutano wa hadhara uliofanyika katika kijiji cha Qangded, kilichopo katika hiyo.

Akizungumza katika mkutano huo, Kubenea alimuomba Lissu ambaye wakati huo kuongea na wananchi wa kata hiyo ambayo ilikuwa inaongozwa na marehemu Thomas Moshi Darado. Lissu alikubali ombi hilo.

“…hapa nilipo niko na shujaa wa taifa hili, Mheshimiwa Tundu Lissu, ambaye nyote mnajua kilichompata. Yuko kwenye matibabu nje ya nchi. Anaomba kuzungumza na ninyi,” alisema Kubenea huku akishangiliwa na wananchi.

Naye Lissu akihutubia mkutano huo kwa njia ya simu aliwataka wananchi wa Qangded, kumchagua mgombea wa Chadema, Dagharo Hamay Kisimbi kwa maelezo kuwa ndiye mwenye sifa ya kufuata nyayo za diwani aliyekuwapo.

Alisema, “ndugu zangu wa kata ya Baray, mimi naitwa Tundu Lissu. Ninaongea kutoka nchini Ubelgiji ambako nimekuja kutibiwa. Kama ningekuwa na afya nzuri, basi leo ningekuwa nanyi hapo Baray.

“Mnajua kuwa marehemu  Tomas Darabe alikuwa rafiki yangu mkubwa. Hivyo basi, kwa heshima yake na heshima yangu kwenu, nawaomba sana mumchague diwani wa Chadema, ” alieleza.

Alisema, “katu wananchi wa Karatu, msikubali kurudishwa utumwani na CCM. Msikubali. Ninawaomba muendelee kutuunga mkono ili tuweze kuwahudumia.”

Kwa upande wake Kubenea alirejea kauli yake kuwa hana mapngo wa kuondoka Chadema na kuongeza kuwa wanaoeneza habari hiyo, “wanapaswa kupuuzwa.”

Alisema, “ndugu zangu nchi hii imejaa uonevu na njia pekee iliyosalia ya kuondoa uonevu huo na unyanyasaji, ni kukiondoa  Chama Cha Mapinduzi, madarakani.

“Nasikia watu wanasema nataka kujiunga na CCM. mimi siyo mtu wa kutanganga na wala siwezi kujiunga na chama kinachohubiri amani, lakini kikiwa kinatenda uhalifu.”

Aliwataka wananchi kumuenzi marehemu Darabe kwa kumchagua diwani  anayetokana na chama chake na ambaye kweli atakuwa mwakilishi wa wananchi.

Alisema, madai kuwa Chadema itashinda uchaguzi huo, lakini CCM ndio watakaotangazwa mshindi, hayana nafasi katika kata hiyo; yeye binafsi atakuwapo Karatu siku ya uchaguzi kuhakikisha mgombea wao anatangazwa mshindi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari MchanganyikoTangulizi

Afya ya akili yatajwa chanzo kuvunjika ndoa

Spread the loveCHANGAMOTO ya afya ya akili, imetajwa kuwa chanzo cha migogoro...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

error: Content is protected !!