Friday , 2 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea: Nilihofia kugawa kura Ubungo
Habari za Siasa

Kubenea: Nilihofia kugawa kura Ubungo

Spread the love

SAED Kubenea, mgombea ubunge katika Jimbo la Kinondoni kupitia Chama cha ACT-Wazalendo, amesema hakugombea ubunge katika Jimbo la Ubungo ili kutogawa kura za upinzani. Anaripoti Hamis Mguta, Dar es Salaam … (endelea).

Akizungumza kwenye uzinduzi wa kampeni za mgombea udiwani kwenye Kata ya Tandale, jimboni humo Mohammed Ismail, tarehe 13 Septemba 2020 amesema, hayupo radhi kugawa kura za upinzani.

”Nimefikia uamuzi wa kuacha kugombea Ubungo kwasababu  ningeng’ang’ania kugombea, ningegawa kura na hatimaye CCM ishinde, sitaki kushiriki dhambi hiyo,” amesema Kubenea na kuongeza:

“Nimegombea Kinondoni kwa kuwa, naijua vizuri na nimeshiriki shughuli nyingi nikiwa kwenye Manspaa ya Kinondoni kwa mwaka mmoja na nusu.”

Amesema, ataendelea kutetea ajenda za wananchi na kwamba atahakikisha anamaliza athari za mafuriko katika jimbo hilo.

Amesisitiza kwamba, licha ya kufanyiwa vitimbi na hata kumwagiwa tindikali usoni wakati akiwatetea wananchi kupitia kalamu yake, hajawahi kuusaliti umma.

1 Comment

  • “Разум, однажды расширивший собственные границы, никогда не воротится в бывшие.” – доказывал А. Эйнштейн. Превеликое спасибо только за то, что Вы, своими заметками, позволяете разуму перейти за пределы привычных границ.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

Habari za SiasaTangulizi

Zanzibar watangaza rasmi kuwa shamba la Razaba ni mali yao

Spread the love  SERIKALI ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), imetangaza rasmi kwamba shamba...

Habari za SiasaTangulizi

Rais Mwinyi azindua Kamati ya Maridhiano Visiwani

Spread the love  RAIS wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), Dk. Hussein...

error: Content is protected !!