Tuesday , 5 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea, Komu waanza kuhojiwa na Kamati Kuu Chadema
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea, Komu waanza kuhojiwa na Kamati Kuu Chadema

Anthony Komu Mbunge wa Moshi Vijijini na Saed Kubenea wa Ubungo
Spread the love

WABUNGE Saed  Kubenea (Ubungo) na Anthony Komu (Moshi Vijijini) wameanza kuhojiwa na Kamati Kuu ya Chadema katika kikao cha kamati hiyo kinachoendelea leo Jumatano Oktoba 17, 2018 katika ukumbi wa Ledger Plaza katika Hoteli ya Bahari Beach. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kikao hicho pamoja na ajenda nyingine lakini pia kimekutana kuwajadili wabunge hao wawili baada ya kudaiwa kupanga mpango hasi dhidi ya Meya wa Ubungo, Boniface Jacob kupitia kile kinachodaiwa sauti iliyotengeneza ya mpango huo.

Kubenea na Komu katika siku za hivi karibuni wamezua mjadala ndani na nje ya chama hicho baada ya kuvuja kwa sauti hiyo ambayo inadaiwa ni mazungumzo kati ya wabunge hao.

Wabunge hao waliwasili ukumbi hao majira ya saa 8:01 mchana ambapo baada ya kupewa maelezo, Komu ndiyo alikuwa wa kwanza kuingia kuhojiwa mbele ya kamati hiyo huku Kubenea akisubiri muda wake kuitwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko: Viongozi tuache alama nzuri katika utendaji wetu

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Chanzo maporomoko yaliyoua 65 Hanang, chatajwa

Spread the loveSERIKALI imesema kumeguka kwa sehemu ya Mlima Hanang ambao ilikuwa...

Habari za Siasa

Baba yake Ole Sabaya ashinda Uenyekiti CCM – Arusha

Spread the loveLoy Thomas Sabaya ambaye ni Baba wa aliyekuwa Mkuu wa...

Habari za Siasa

Serikali yaagiza uchunguzi chanzo maporomoko Hanang

Spread the loveSERIKALI imeagiza uchunguzi ufanyike ili kubaini chanzo cha maporomoko ya...

error: Content is protected !!