Tuesday , 3 October 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea awachonganisha wabunge wa CCM na JPM
Habari za SiasaTangulizi

Kubenea awachonganisha wabunge wa CCM na JPM

Spread the love

MBUNGE wa Ubungo (Chadema), Saed Kubenea, ameweka rehani mshahara wake wa mwezi huu, ikiwa Leo jioni wabunge wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), wataweza kuzuia bajeti ya wizara ya Kilimo na Uvuvi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza kwa hisia kali wakati akichangia bajeti ya wizara hiyo, Kubenea amesema, “hakuna mbunge hata mmoja ambaye anaweza kuzuia bajeti.”

Amesema, wabunge wa chama hicho ni dhaifu na hawana uwezo wa kusimamia mambo yao mpaka mwisho.

“Mheshimiwa Spika kama atasimama mbunge yeyote wa CCM na kutaka kukwamisha bajeti hii, natangaza mshahara wangu wa mwezi huu apewe akaongezee bajeti yake, huwa mnatupiga maneno tu bila vitendo,” amesema Kubenea.

Kubenea ametoa kauli hiyo leo bungeni katika mjadala wa bajeti hiyo, kubainisha kuwa wabunge wa CCM wamekuwa wakipitisha kwa nguvu bajeti baada ya kuitwa kwenye vikao vya ndani vya chama hicho.

Baada ya Kubenea kueleza hayo, baadaye Spika wa Bunge, Job Ndugai aliwatangazia wabunge  wa chama hicho tawala kuwa watakuwa na kikao cha ndani kitakachofanyika katika ukumbi wa White House, kabla ya kurejea tena bungeni saa 10 jioni.

Mara nyingi hoja za wabunge zinapokuwa moto bungeni kuhusu wizara fulani, CCM huitisha vikao hivyo vya ndani.

Amesema ni aibu kwa Serikali kuendelea kuagiza nyama, kuku na samaki kutoka nje ya nchi wakati vitu hivyo vimejaa nchini.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania, kesho tarehe 3 Oktoba 2023, inatarajia...

Habari MchanganyikoTangulizi

Mobhare Matinyi Msemaji mpya wa Serikali

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua aliyekuwa Mkuu wa...

Habari MchanganyikoTangulizi

Basi la Magereza lagonga treni yenye abiria 650 Dar

Spread the loveBasi  Jeshi la Magereza lenye namba MT 0040 limegonga treni...

error: Content is protected !!