Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea amchongea Tarimba kwa wanakinondoni
Habari za Siasa

Kubenea amchongea Tarimba kwa wanakinondoni

Spread the love

SAED Kubenea, mgombea Ubunge Kinondoni jijini Dar es Salaam kupitia ACT-Wazalendo, amemchomgea Abbas Tarimba, mgombea ubunge jimbo hilo wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) kwa wananchi ili wasimchague. Anaripoti Mwandishi Wetu, Kinondoni … (endelea).

Kubenea amewaomba wananchi wa Kinondoni kutomchagua Tarimba katika Uchaguzi Mkuu utakaofanyika Jumatano tarehe 28 Oktoba 2020 kwa maelezo atakwenda kutekeleza masilahi ya chama chake badala ya wananchi watakaomtuma.

Mgombea huyo ubunge wa ACT-Wazalendo ametoa kauli hiyo jana Ijumaa tarehe 25 Septemba 2020 katika mkutano wa kampeni uliofanyika Kigogo jijini Dar es Salaam.

Kubenea alisema, wakati Tarimba akiwa Diwani wa Hananasif wilayani Kinondoni, aliungana na msimamo wa CCM wa kutolipa fidia wananchi waliotakiwa kubomolewa makazi yao kwa ajili ya kupisha miradi ya ujenzi wa barabara na upanuzi wa Mtoa wa Ng’ombe.

“CCM wanapewa fedha na Benki ya Dunia kujenga barabara na kupanua Mto wa Ng’ombe kutoka Chuo Kikuu wakasema hatuwezi kulipa fidia hili zoezi mfanye wenyewe.”

“CCM wakakataa kulipa fidia sisi wana Ukawa katika Baraza la Madiwani tukapitisha azimio katika mradi huu wananchi walipwe fidia,” alisema Kubenea.

Kubenea aliyekuwa mbunge wa Ubungo kupitia Chadema alisema, wakati Halmashauri ya Wilaya ya Kinondoni haijagawiwana kuwa na halamshauri mbili ya Ubungo na Kinondoni, madiwani wa CCM walipingana na madiwani wa upinzani ambao walikuwa wanapigania wananchi wapewe fidia.

Hata hivyo, Kubenea alisema Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kwa kushirikiana na Chama cha Wananchi (CUF) vilikuwa vinaongoza halmashauri hiyo, vilipitisha azimio la kukopa fedha katika Benki ya CRDB kulipa fidia wananchi ili Benki ya Dunia (WB) itoe fedha za utekelezaji wa mradi huo.

“Tukaenda benki ya CRDB tukakopa fedha kwa ajili ya kulipa fidia wananchi wa Kinondoni, bila sisi msingelipwa fidia sababu jambo lile lilisimamiwa na Serikali Kuu lakini sisi tuliamua kulipa fidia.”

“Hiyo kazi yetu ya kwanza tuliifanya Kinondoni ambapo Tarimba akiwa diwani wa CCM alikataa kulipa fidia aje hapa aseme kwamba sio kweli,” alisema Kubenea.

Akizungumzia ahadi zake, Kubenea aliwaomba wananchi wa Kinondoni wamchague kwa kuwa atamaliza tatizo la mafuriko ndani ya miaka mitano.

Kubenea alisema ataiomba Benki ya Dunia fedha za upanuzi wa Mto Msimbazi na Mto wa Ng’ombe.

“Ukiwa na mbunge anayejua kazi yake, maendeleo lazima yapatikane. Kinondoni kuna tatizo la mafuriko, nawaambia ndani ya miaka mitano nitalimaliza kwani kuna fedha za Benki ya Dunia za kupanua Mto Msimbazi wao wanawaita mabeberu lakini sisi tutakwenda kuwapigia magoti kuomba fedha za upanuzi huo,” ameahidi Kubenea.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

error: Content is protected !!