Tuesday , 23 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kubenea akagua ukarabati wa shule
Habari za Siasa

Kubenea akagua ukarabati wa shule

Spread the love

SAED Kubenea, Mbunge wa Ubungo (Chadema), amefanya ziara ya ukaguzi wa ukarabati wa Shule za Msingi Mabibo na Makuburi zilizopo jimboni mwake, anaandika Faki Sosi.

Shule hizo zinakarabatiwa kwa fedha kutoka Halmashauri ya Ubungo na mfuko wa mbunge huyo ambazo zote zinakaribia kufikia Sh. 90 milioni.

Mfuko wa mbunge umetoa Sh. 17 milioni kwa ajili ya kukarabati shule ya msingi Makuburi.

Ukarabati huo ni wa majengo matano ya Shule ya Mabibo inayowekwa mabati mapya kutoka vigae ambavyo vimeharibika gharama yake ni Sh. milioni 17 kutoka mfuko wa jimbo wa Mbunge na ukarabati wa madarasa Shule ya Makuburi Sh. 40 milioni na Sh. 32 milioni zinazotumika kujenga vyoo.

Katika ziara hiyo, Kubenea aliambatana na Ofisa Mtendaji Kata ya Makuburi na Mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa ya Mwongozo zilipo shule hizo mbili pamoja na wajumbe wa Kamati za Shule.

Kubenea ametembelea darasa la tatu la Shule ya Makuburi na kuwaahidi wanafunzi watano watakaofanya vizuri katika mtihani wao wa taifa wa darasa la nne mwakani atawazawadi Sh. 100,000 kila mmoja.

Wakati huo huo Kubenea amewasalimu walimu wa shule hizo pamoja na wanafunzi hao ambao amewasisitiza kusoma kwa bidii ili siku moja waje wawe wabunge, walimu, wanasheria na wahandisi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali kuanzisha mradi wa Gridi ya maji ya Taifa

Spread the loveWaziri wa Maji, Jumaa Aweso amesema katika mwaka wa fedha...

Habari za Siasa

Rais Samia aridhishwa utendaji mabalozi, awapa neno

Spread the loveRais wa Tanzania, Dk. Samia Suluhu Hassan amewapongeza mabalozi  wanaowakilisha ...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

NMB yadhamini Mkutano Mkuu ALAT, kufunguliwa na Samia

Spread the loveBENKI ya NMB, imekabidhi hundi yenye thamani ya Sh. 120...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mipango na uwekezaji kutumia bilioni 121.3, mradi wa Bagamoyo wapewa kipaumbele

Spread the loveWIZARA ya Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji, imeliomba Bunge...

error: Content is protected !!