Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Kuagwa Mkapa: Ndege ya mwakilishi Kenya, yashindwa kutua Tanzania
Habari Mchanganyiko

Kuagwa Mkapa: Ndege ya mwakilishi Kenya, yashindwa kutua Tanzania

Profesa Palamagamba Kabudi
Spread the love

NDEGE iliyombeba mwakilishi wa Kenya, Samuel Poghisio aliyekuwa anakwenda Tanzania, kuhudhuria shughuli ya kitaifa ya kumuaga Hayati Benjamin Mkapa, Rais wa Awamu ya Tatu, imelazimika kurejea Kenya. Anaripoti Mwandishi Wetu, Dar es Salaam … (endelea).

Taarifa ya mwakilishi wa Uhuru Kenyatta, Rais wa Kenya kushindwa kufika kwenye shughuli hiyo leo Jumanne tarehe 28 Julai 2020, imetolewa na Profesa Palamagamba Kabudi, Waziri wa Mambo ya Nje wa Tanzania.

Akizungumza kwenye shughuli hiyo leo Jumanne katika Uwanja wa Uhuru, jijini Dar es Salaam, Prof. Kabudi amesema, mpaka sasa (ilikuwa asubuhi) hawajapata taarifa kutokana na ndege hiyo kulazimika kurudi Kenya kabla ya kutua Tanzania kama ilivyokusudiwa.

Kwenye shughuli hiyo, Jenerali Alain Guillaume ambaye ni Waziri Mkuu wa Burundi, amefikisha salamu za rambirambi za rais wa taifa hilo Jenerali Evariste Ndayishimiye.

Samuel Poghisio

Amesema, Rais Ndayishimiye na Burundi yote wanawafariji Watanzania katika kipindi hiki kigumu, “muhimu ni tueendelea kumuombea Hayati Mkapa.”

Mwili wa Mpaka ulikuwa unaagwa kitaifa uwanjani hapo na kuongozwa na Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli.

Mkapa alifariki dunia Alhamisi tarehe 23 Julai 2020 saa 3:30 usiku kwa mshtuko wa moyo. Mwili wake, utazikwa kesho Jumatano kijijini kwake, Lupaso, Masasi Mkoa wa Mtwara.

Endelea kufuatilia MwanaHALISI Online, MwanaHALISI TV na mitandao yetu ya kijamii kwa habari na taarifa mbalimbali

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

error: Content is protected !!