
Rais Jakaya Mrisho Kikwete (kulia) akitoka ndani ya nyumba ya mfano baada ya kuzindua nyumba za gharama nafuu za NHC Mnyakongo zilizopo Kongwa mkoani Dodoma
WANANCHI wa Mji mdogo wa Kibaigwa Wilaya ya Kongwa mkoani Dodoma, watajengewa uwezo wa kutafuta taarifa na kuzichambua ili waweze kufuatilia na kusimamia mipango ya bajeti na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kijamii na kiuchumi katika maeneo yao. Anaandika Dany Tibason, Kongwa …. (endelea).
Mkurugenzi wa Asasi ya Afya ya Jamii Tanzania (AJAT), yenye makao yake katika Mji mdogo wa Kibaigwa, Abdallah Mbwasi amesema mradi huo utatekelezwa kwa miaka mitatu unatarajia kukamilika Februari 2018.
“Lengo la mradi ni kuwajengea wananchi uwezo wa kutafuta taarifa na kuzichambua ili waweze kufuatilia na kusimamia mipango ya bajeti na utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kijamii kiuchumi katika maeneo yao” amesema.
Amewataka wananchi kuupokea mradi huo kwani utakuwa na manufaa kwao kwani kujengewa uwezo hupelekea kuamsha mambo mengi ambayo walikuwa hawayafahamu ikiwemo suala la ufuatiliaji wa bajeti.
Amesema elimu hiyo itawafanya wananchi wawe hata na uwezo wa kuhoji na kufuatilia taarifa za mapato na matumizi kwenye maeneo yao.
Amesema mradi huo utatekelezwa kwa kushirikisha Asasi tatu ikiwemo Afya ya Jamii Tanzania ambayo itahusisha kata ya Kibaigwa na Ndurugumi, Asasi ya AFNET itatekeleza mradi katika Kata ya Ugogoni na Mkoka na Asasi ya Umwema ambayo itatekeleza mradi katika Kata ya Mlali na Chamkoroma.
Aidha, amesema mradi huo utawajengea uwezo wananchi kudai uwajibikaji na utawala bora katika utoaji wa huduma bora za afya.
Mbwasi amesema mradi utaendesha semina juu ya ufuatiliaji na uwajibikaji jamii kwa viongozi wa seruikali ya mtaa, kamati za usimamizi na uendeshaji za zahanati za Kibaigwa na Ndurugumi.
Mradi huo umefadhiliwa na TACOSODE kwa msaada wa Watu wa Marekani.
More Stories
Bashungwa atoa maagizo 10 kwa waajiri na waajiriwa wapya
Gesi asilia kuinua uchumi wa wananchi
Watu 17 wafariki dunia kwa mkanyagano ‘Night Club’