Wednesday , 24 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kongamano la Chadema kudai katiba mpya njia panda
Habari za SiasaTangulizi

Kongamano la Chadema kudai katiba mpya njia panda

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

 

KONGAMANO la kudai katiba mpya, lililoandaliwa na Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), liko njia panda baada ya Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Robert Gabriel, kupiga marufuku mikusanyiko. Anaripoti Mwandishi Wetu, Mwanza…(endelea).

Kongamano hilo lilipangwa kufanyika kesho tarehe 21 Julai 2021, jijini Mwanza, baada ya kuzuiwa mara ya kwanza, tarehe 16 Julai mwaka huu.

Akizungumza na wanahabari leo tarehe 20 Julai 2021, Gabriel amesema lengo la marufuku hiyo ni kudhibiti maambukizi ya ugonjwa wa homa kali ya mapafu, inayosababishwa na Virusi vya Corona (Covid-19).

Mkuu wa mkoa huyo wa Mwanza, ameelekeza wilaya zote jijini humo, kutotoa vibali kwa matukio na mikusanyiko, aliyoita siyo ya lazima.

John Mrema, Mkurugenzi wa Mawasiliano, Itikadi, Uenezi na Mambo ya Nje wa Chadema

“Niendelee kusihi matukio ambayo sio ya dharura , sipendelei na nitoe wito kwa maneo ya wilaya zote, waangalie na wafanye tathimini. Kuna mambo ambayo naona sio ya lazima haina haja kuruhusu, ambayo yataleta madhara kwa watu bila sababu yoyote,” amesema Gabriel.

Aidha, Gabriel amewaeleza wageni waliopanga kwenda jijini humo kufanya matukio mbalimbali, kwamba mkoa huo uko katika kampeni ya kupambana na Covid-19.
“Nisihi tena kwamba, mikusanyiko isiyokuwa na sababu, kipindi hiki hatuna sababu ya kutoa vibali na niwatahadharishe hata wanaokuja Mwanza kwa ajili ya matukio makubwa, tuko kwenye kampeni kubwa,” amesema Gabriel.

Kongamano hilo la Chadema la kudai katiba mpya, lililoandaliwa na baraza la vijana la chama hicho (Bavicha), lilipangwa kufanyika Jumamosi iliyopita, lakini lilishindikana baada ya kukosa kibali.

MwanaHALISI Online ilimtafuta Mkurugenzi wa Itifaki na Mambo ya Nje Chadema, John Mrema, ili kujua hatma ya kongamano hilo, ambaye amesema chama hicho kitatoa tamko kuhusu suala hilo.

Hata hivyo, Mrema amesema “kiufupi yeye hajamtaka kwamba amezuia kongamano la katiba, sisi tunaandaa tamko tutalitoa baadae.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!