Wednesday , 29 March 2023
Home Gazeti Habari Mchanganyiko Kondoa walia na miundombinu mibovu ya maji
Habari Mchanganyiko

Kondoa walia na miundombinu mibovu ya maji

Spread the love

WAKAZI wa kata ya Chemchem wilaya ya Kondoa mkoani Dodoma wameiomba serikali kuwatatulia kero ya muda mrefu ya uchakavu wa  miundombinu ya mabomba ya maji ambayo toka yawekwe mwaka 1961 hayajafanyiwa ukarabati wowote. Anaripoti Dany Tibason, Dodoma … (endelea).

Wakizungumza na vyombo vya habari kwa nyakati tofauti kuhusiana na kero hiyo, Mariam Said mkazi wa mtaa wa Iboni pamoja na Abuu Mwenda wa mtaa wa Chemchem, walisema kuwa kutokana na uchakavu huo mabomba hayo hivi sasa yanakutu na yaliyo mengi yamepasuka na kusababisha upotevu wa maji.

Mariam ambaye ni mkazi wa mtaa wa Chemchem alisema kuwa uchakavu wa miundombinu hiyo ya mabomba kwa upande wao imewasababishia kukosa hata na huduma ya maji kutokana na yaliyo mabomba yake yametoboka na hata yakitoa maji upotea.

“Hivyo tunaiomba serikali yetu sikivu kulishughulikia jambo hili ya ukarabati wa hii miundombinu ya mabomba ambayo toka yamewekwa mwaka 1961 mpaka leo hii hayajafanyiwa ukarabati na hata maji yake yamekuwa yakitoka kwa shida mno,” alisema Mariam.

Naye Abuu Mwenda alisema kuwa kuwepo kwa uchakavu huo wa mabomba wa muda mrefu kuna kila sababu kuwa tumekuwa tukinywa maji ambayo siyo salama kwa afya kwa kuwa yaliyo mengi yamechokaa na kushikwa na kutu.

Hata hivyo mkazi huyo alisema kuwa kwa hivi sasa huduma hiyo tunaipata kwa wiki mara mbili kwenye kata hiyo,suala ambalo linatulazimisha kutumia maji yanayopatikana kwenye mto wa chemchem ambayo hata hivyo siyo salama pia.

Akizungumza kuhusiana na kero hiyo Diwani wa kata hiyo Kipaya Mdachi alikiri kuwepo kwa shida hiyo ya mabomba ambayo yaliyowekwa katika kipindi cha upatikanaji wa uhuru wan nchi hii.

“Mimi nikiwa Diwani wa kata hii Chemchem ambayo nina mitaa yangu minne ikiwemo mtaa wa Uboni, Ubembeni,  Chemchem na Kwa Pakacha, tatizo hilo la uchakavu wa mabomba ni kweli lipo na wananchi wangu wamekuwa wakikosa maji salama kutokana na miundombinu hiyo uchakavu,” alisema.

Mdachi alisema hata hivyo anaamini serikali kwa kupitia kilio hicho cha wananchi watatengewa fedha kwa ajili ya kufanyiwa ukarabati huo wa mabomba hayo ambayo hivi sasa hana sifa ya kuweza kahudumia maji yaliyo salama kwa wanadamu.

Diwani huyo alisema kutokana na kero hiyo kwa upande wake anaiomba serikali kuwachimbia visima ambavyo vitakavyowasaidia kwa hivi sasa katika upatikanaji wa maji salama wakati ukidanyiwa mchakato wa kufanyika kwa ukarabati wa mabomba hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Rais Samia awataka wahariri kufanya kazi bila uoga, upendeleo

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan amewataka wahariri wa vyombo...

Habari Mchanganyiko

STAMICO yasaini mkataba wa bilioni 55.2 kuchoronga miamba GGML

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limezidi kufanya vizuri katika...

Habari Mchanganyiko

NMB yatoa traksuti za Mwenge wa Uhuru Mtwara

Spread the loveBENKI ya NMB imetoa traksuti kwa mkoa wa Mtwara ambako...

Habari Mchanganyiko

Yara yaja na bima ya mazao kwa wakulima

Spread the love  WAKATI serikali ikiweka mikakati mbalimbali kuimarisha sekta ya kilimo...

error: Content is protected !!