Thursday , 30 March 2023
Home Kitengo Habari Siasa Kodi taulo za kike: Zitto ajenga hoja
SiasaTangulizi

Kodi taulo za kike: Zitto ajenga hoja

Spread the love

ZITTO Kabwe, Kiongozi Mkuu wa Chama cha ACT-Wazalendo, amepinga pendekezo la serikali la kurejesha Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT), kwenye taulo za kike. Anaandika Mwandishi Wetu…(endelea).

Mwanasiasa huyo mashuhuri leo tarehe 21 Juni 2019 bungeni amesema, serikali imefanya haraka kurejesha kodi hiyo huku ikishindwa kuchukua mfano wa mwaka jana wa kupandisha kodi ya mafuta ghafi kutoka nje, ili kulinda viwanda vya ndani ambapo licha ya kutoonesha matokeo, bado imejipa muda.

Kwa mfano huo Zitto ambaye ni Mbunge wa Kigoma Mjini amesema, serikali imefanya haraka kurejesha VAT kwenye taulo hizo kinyume na mapendekezo yake ya mwaka wa fedha 2018/19 ya kuondoa kodi hiyo.

Akisoma makisio ya Mapato na Matumizi kwa Mwaka wa Fedha 2019/20 tarehe 13 Juni 2019, Dk. Philip Mpango, Waziri wa Fedha na Mipango alisema, serikali imependekeza kurejeshwa kwa kodi hiyo kwa kuwa, kuondoa kodi hiyo hakukupunguza bei ya taulo hizo.

Hata hivyo Zitto amesema, serikali haikupaswa kupima matokeo ya kuondoa kodi hiyo kwa mwaka mmoja na kwamba, wakati kodi hiyo inaondolewa wafanyabiashara wengine walikuwa na mzigo ndani hivyo wasingeweza kupunguza.

Lakini pia amesema, bei hiyo inaweza kuwa imebaki palepale kutokana na shilingi ya Tanzania kuyumba kwa kuwa, taulo hizo nyungi zinatoka nje hususan Marekani.

“Serikali inapaswa kutafakati kwamba, je mwaka mmoja ambao utekelezaji umefanyika, unatosha kipimo sahihi?” amehoji Zitto na kuongeza “kodi imeanza Julai 2018 ambapo kulikuwa na watu wana bidhaa ambazo walinunua hazikuwa na punguzo hilo, lazima watauza kwa bei ile ile.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Rais Samia ampandisha cheo RPC wa Dar

Spread the loveMKUU wa Jeshi la Polisi nchini (IGP), Camillus Wambura, amesema...

Habari za SiasaTangulizi

Wanachama 384 CUF watimkia Chadema, Mbowe awapokea, Kambaya ndani…

Spread the loveJUMLA ya wanachama 384 wanachama wa Chama cha Wananchi CUF...

Habari za SiasaTangulizi

Mawakili wa Chadema wabadilishia gia angani

Spread the loveMAWAKILI wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), wameiomba Mahakama...

Habari za SiasaTangulizi

Mbunge Jesca Kishoa avunja ndoa na Kafulila

Spread the love  NDOA baina ya Jesca David Kishoa, mbunge wa Viti...

error: Content is protected !!