Sunday , 3 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kuchomwa ofisi za Chadema: Polisi waingia mtaani
Habari za Siasa

Kuchomwa ofisi za Chadema: Polisi waingia mtaani

Salumu Hamduni, Mkurugezni Mkuu wa TAKUKURU
Spread the love

WATU waliohusika na tukio la kuchoma Ofisi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Kaskazini, sasa wanasakwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea).

Jeshi la Polisi Arusha limeeleza, kwamba lipo kwenye msako na uchunguzi kwa watu waliohusika na tukio hilo likieleza samani zilizokuwa kwenye ofisi hizo ziliteketea.

“Ni kweli ofisi zilivamiwa na kufayiwa uharibifu. Tunawasaka na tutawachukulia hatua,” amesema Salumu Hamduni, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha.

Taarifa kutoka Arusha zinaeleza, usiku wa kuamkia tarehe 14 Agosti 2020, ofisi hizo zilishambuliwa na kuteketea kwa moto. Polisi wanasema ‘waliohusika hawajajulikana.

Kamanda Hamdan anasema, watu waliohusika wakikamatwa, sheria zitachukua mkondo wake. Ofisi hiyo ipo katika Kata ya Kimandolu, jijini humo.

Shambulizi kwenye ofisi hiyo zilisababisha hasara na uharibifu wa mali mbalimbali ikiwamo kuvunjwa kwa vioo vya madirisha sita. Bado thamani kamali ya uharibifu haijajulikana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Dk. Biteko aagiza wakurugenzi TANESCO kukemea rushwa kwenye maeneo yao

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Uongozi wa Samia kuendelea hadi 2030

Spread the loveKWETU sisi tuliowahi kusoma sekondari, iwe O levo au A...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Bado askari wastaafu wanaonewa

Spread the loveRAIS wangu Samia Suluhu Hassan tunaendelea kumshukuru Mungu kwamba wote...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Tunastawisha ufisadi na kuchukia matunda yake

Spread the loveBUNGE la Jamhuri linaloendelea mjini Dodoma, kwa wiki nzima limetawaliwa...

error: Content is protected !!