Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kuchomwa ofisi za Chadema: Polisi waingia mtaani
Habari za Siasa

Kuchomwa ofisi za Chadema: Polisi waingia mtaani

Salumu Hamduni, Mkurugezni Mkuu wa TAKUKURU
Spread the love

WATU waliohusika na tukio la kuchoma Ofisi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) Kanda ya Kaskazini, sasa wanasakwa. Anaripoti Mwandishi Wetu, Arusha…(endelea).

Jeshi la Polisi Arusha limeeleza, kwamba lipo kwenye msako na uchunguzi kwa watu waliohusika na tukio hilo likieleza samani zilizokuwa kwenye ofisi hizo ziliteketea.

“Ni kweli ofisi zilivamiwa na kufayiwa uharibifu. Tunawasaka na tutawachukulia hatua,” amesema Salumu Hamduni, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Arusha.

Taarifa kutoka Arusha zinaeleza, usiku wa kuamkia tarehe 14 Agosti 2020, ofisi hizo zilishambuliwa na kuteketea kwa moto. Polisi wanasema ‘waliohusika hawajajulikana.

Kamanda Hamdan anasema, watu waliohusika wakikamatwa, sheria zitachukua mkondo wake. Ofisi hiyo ipo katika Kata ya Kimandolu, jijini humo.

Shambulizi kwenye ofisi hiyo zilisababisha hasara na uharibifu wa mali mbalimbali ikiwamo kuvunjwa kwa vioo vya madirisha sita. Bado thamani kamali ya uharibifu haijajulikana.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Wabunge waikalia kooni TAKUKURU Bungeni

Spread the love  BAADHI ya wabunge wamelia na changamoto za utendaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Mpina ataka Waziri Majaliwa ajiuzulu, akosoa teuzi za mawaziri

Spread the love  MBUNGE wa Kisesa, Luhaga Mpina, amemtaka Waziri Mkuu, Kassim...

Habari za Siasa

CCM yakemea ufisadi, yaipa kibarua TAKUKURU

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimekemea vitendo vya ubadhirifu wa...

Habari za Siasa

Bajeti ya Ikulu 2024/25 kuongezeka, bunge laombwa kurudhia Sh. 1.1 trilioni

Spread the love  WIZARA ya Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa...

error: Content is protected !!