TIMU ya Mtibwa Sugar ya Morogoro nchini Tanzania, imemtambulisha Omog Joseph Marious (49), raia wa Cameroon kuwa kocha mkuu wa timu hiyo. Anaripoti Mitanga Hunda, TUDARCo … (endelea).
Omog aliyewahi kuzifundisha timu za Simba na Azam FC za Tanzania kwa nyakati, ametambulishwa jana Ijumaa, tarehe 24 Septemba 2021.
Katika kurasa zake za kijamii cha Mtibwa, wamewekwa picha za Omog na kuandika “tunayofuraha kumtambulisha kwenu kocha wetu mpya Omog Joseph Marious.”
“Ujuzi wake ukichanganya na ujuzi wa kikosi chetu na sukari yetu bora nchini mambo yatakuwa matamu sanaaa..!.”
Omog aliifundisha Simba kwa mwaka mmoja katika msimu wa 2016/17 akianza Azam FC yenye makazi yake Chamanzi-Mbagala jijini Dar es Salaam kati ya 2013 hadi 2015.
Leave a comment