Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Kocha wa Samatta atimliwa Aston Villa
Michezo

Kocha wa Samatta atimliwa Aston Villa

Spread the love

 

TIMU ya Aston Villa inayoshiriki Ligi Kuu ya Uingereza, imemfukuza kazi kocha wake mkuu, Dean Smith. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Smith (50) aliyejiunga na Villa Oktoba 2018, amefukuzwa leo Jumapili, tarehe 7 Novemba 2021, baada ya mwenedo wa timu hiyo katika ligi kuwa mbaya.

Kati ya michezo 11 iliyocheza, imejikusanyia pointi 10 pekee ikiwa nafasi ya 15 kati ya timu 20 zinazoshiriki ligi hiyo.

“Msimu huu, hatujaona mabadiliko ya timu, matokeo mazuri na nafasi tulipo kwenye ligi si mzuri. Kutokana na sababu hizo, tumeamua kufanya mabadiliko ili aje kocha mpya,” amesema Christian Purslow, Ofisa wa timu hiyo

Smith, atakumbukwa na Watanzania wengi, baada ya kuwezesha Mtanzania wa kwanza, Mbwana Samatta kucheza Ligi Kuu ya Uingereza (EPL).

Samatta ambaye ni nahodha wa kikosi cha soka cha Tanzania ‘Taifa Stars’ anayecheza nafasi ya ushambuliaji, alisajiliwa na Aston Villa, Januari 2020 akitokea KRC Genk ya nchini Ubelgiji.

Kabla ya kutua Villa Park, Samatta alicheza kwa misimu minne KRC kuanzia mwaka 2016-2020 akitokea TP Mazembe ya Congo.

Hata hivyo, Samatta hakuwa na wakati mzuri ndani ya kikosi hicho cha Smith na Septemba 2020, alipelekwa kwa mkopo Fenerbahce ya Uturuki.

Septemba 2021, Samatta alirejea kwa mara nyingine Ubelgiji na safari hii akijiunga kwa mkopo na Royal Antwerp inayoshiriki ligi kuu nchini humo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!