Friday , 29 March 2024
Home Kitengo Michezo Kocha Simba: Yanga walikuwa wanazuia
Michezo

Kocha Simba: Yanga walikuwa wanazuia

Spread the love

KOCHA wa Simba, Sven Vandebroeck amesema “kuLikuwa  na timu moja inacheza mpira na nyingine inazuia, nawapongeza wachezaji wangu kwa kucheza vizuri na ninafuraha kwa kile walichokionesha.” Anaripoti Kelvin Mwaipungu, Dar es Salaam … (endelea).

Sven amesema hayo mara baada ya kumalizika kwa mchezo kati ya Yanga dhidi ya Simba uliochezwa kwenye Uwanja wa Mkapa jijini Dar es Salaam.

Aidha kocha huyo ameendelea kusema kuwa kipindi cha kwanza hakikuwa kizuri kwa upande wao kwa sababu kasi ya mchezo ilikuwa chini lakini pia mwamuzi alisababisha kutokea kwa jambo hilo

“Kipindi cha kwanza hatukuwa na hali nzuri na mwamuzi alikuwa anatuzuia mara kwa mara lakini kipindi cha pili tulimiliki kiufundi na nguvu” aliongezea kocha huyo.

Bao la kusawazisha la Simba lilifungwa dakika ta 86 na beki wake raia wa Kenya Josh Onyango kwa mpira wa kona mara baada ya Yanga kutangulia katika dakika 31′ kwa bao lilifungwa na Michael Sarpong kwa njia ya penati.

Kwa matokeo haya Simba itaendelea kubakia nafasi ya tatu ikiwa na alama 20 nyuma ya Yanga yenye pointi 24 kwenye nafasi ya pili.

1 Comment

  • Kadi ya mkude kama hakutkana refa Na kuangushwa kwa Luis ilikua Ni njama ya kuichngnya Simba kmchezo

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Makala & UchambuziMichezo

TFF kuamua hatima ya Amrouche

Spread the loveHATIMA ya Kocha Mkuu wa Taifa Stars, Adel Amrouche kuendelea...

Habari za SiasaMichezo

Matinyi: Dk. Ndumbaro alifanya utani ukaguzi mechi za Yanga, Simba

Spread the loveMsemaji Mkuu wa Serikali, Mobhare Matinyi amesema kauli iliyotolewa na...

Michezo

Gethsemane Group Kinondoni (GGK) waachia video ya Bwana Wastahili

Spread the loveWAIMBAJI maarufu nchini kutoka Gethsemane Group Kinondoni (GGK)SDA wameachia video...

BiasharaMichezo

Gamondi kocha bora mwezi Februari, NBC yamjaza manoti

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) ambae ni mdhamini Mkuu...

error: Content is protected !!