Thursday , 25 April 2024
Home Kitengo Michezo Kocha Simba: Tunahitaji kuwa bora ili tupate matokeo
MichezoTangulizi

Kocha Simba: Tunahitaji kuwa bora ili tupate matokeo

Didier Gomes kocha wa Simba
Spread the love

 

MARA baada ya kukubali kichapo cha mabao 4-0, dhidi ya Kaizer Chiefs kocha mkuu wa kikosi cha Simba Didier Gomes ameonekana kutofurahishwa na matokeo na kudai kuwa kama wanataka kufuzu kwenye hatua ijayo wanahitaji kuwa bora zaidi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu…(endelea)

Mchezo huo wa robo fainali ya kwanza Ligi ya Mabingwa Barani Afrika ulipigwa jana kwenye uwanja wa FNB uliopo Johannesburg, nchini Afrika Kusini.

Gomes amefunguka hayo mara baada ya mchezo kumalizika huku akionesha kuwa na matumaini ya kupata matokeo kwenye mchezo ujao ambao utapigwa Jumamosi Tarehe 22 Mei 2021, kwenye Uwanja wa Benjamin Mkapa jijini Dar es Salaam.

“Jambo lolote linawezekana kwenye mpira, hatujafurahia matokeo lakini bado tuna matumaini, ni muhimu sana kuamini kwamba tunaweza kubadili matokeo, lakini kama tunataka kupata matokeo kwenyue mchezo wa marudiano lazima tuwe bora Zaidi,” alisema Gomes

Kwenye mchezo huo wa marudiano Simba inatakiwa kupata ushindi kuanzia mabao 5 na kuendelea bila kuruhusu wavu wao kuguswa.

Kwenye mchezo wa kwanza Kaizer Chiefs walianza kuandika bao la kwanza kwenye dakika ya 6, kupitia kwa Eric Mothoho aliyefunga kwa njia ya kichwa mara baada ya kuunganisha kona na bao la pili lilifungwa na mshambuliaji wao Samir Nurkovic na kufanya mchezo huo kwenda mapumziko Simba ikiwa nyuma kwa mabao 2-0.

Kipindi cha pili kiliporejea Simba ilionekana kumiliki mpira kwa asilimia kubwa hasa eneo la kati kati ya Uwanja, licha ya Kaizer Chiefs kuonekana kuwa na hatari zaidi wanapofika kwenye eneo la mwisho la Simba kwa mashambulizi ya kushtukiza na dakika ya 56 Nurkovic tena aliwaandikia wenyeji hao bao la tatu na kisha dakika ya 63, Leornado Castro akaitimisha kalamau ya bao la nne.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

error: Content is protected !!